Social Icons

Tuesday 8 April 2014

RAIS KIKWETE APONGEZWA

 Bw. Stanley Bergman akiteta jambo na  Balozi Manongi wanaonekana pia wageni waalikwa waliojitokeza kwa wingi kwenye hafla hiyo.
 Rais na Mwanzilishi wa  MCW, Bw. Eddie Bergman akielezea historia ya  Taasisi hiyo ambayo aliianzisha  ( 1999)  akatumia fursa hiyo kutoa shukrani zake kwa wadau , wafadhili na marafiki  mbalimbali ambao wameendelea kuiwezesha  Taasisi hiyo na hatimaye kupitia kwayo kusaidia jamii katika maeneo mbalimbali na uwezeshaji wa  vijana.
 Sehemu ya wageni waalikwa,  aliyekaa mstari wa mbele ni Bw. Ali Velshi  ambaye alikuwa ndiye mshereheshaji wa hafla hiyo. Bw. Velshi    ni mtangazaji maarufu wa  vipindi vya Biashara katika Televisheni ya CNN hivi sasa amehamia Al Jazeera Amerika
 .Bw. Stanley Bergman,  Mwenyekiti na CEO, Henry Schein Inc akizungumza wakati wa hafla ya miaka kumi ya uchangiaji wa Taasisi ya  Miracle Corners of the World ( MCW) ambayo pia imetimiza miaka kumi na tano  ya kuanzishwa kwake,  katika  mazungumzo yake alitoa  shukrani na pongezi kwa Mhe. Rais  Jakaya Kikwete kwa namna ambayo amekuwa akishirikiana na Taasisi hiyo ambayo inaendesha shughuli   hususani   uboreshaji na    uimarishaji wa huduma  ya afya ya kinywa.
 Mhe. Balozi Tuvako Manongi Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akisema machache wakati wa hafla hiyo
Balozi Manongi akiwa na  Mwanamziki Maarufu   Kanda Bongo  Man, kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,  Kanda Bongo  Man alikuwa mmoja wa wageni waalikwa na kama alivyo Balozi Manongi naye pia ni Mwenyekiti wa Heshma wa  MCW

Na Mwandishi Maalum
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete,  ameelezwa  kuwa ni kiongozi ambaye amekuwa akitoa ushirikiano mkubwa kwa  Taasisi  zisizokuwa  za  kiserikali na hivyo kuchagiza kasi ya   taasisi  hizo kuwekeza katika miradi ya kijamii nchini Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa na  Bw. Stanley Bergman,  Mwenyekiti na Mkurugenzi  Mtendaji wa Henry Schein Inc,  wakati wa hafla  ya miaka  kumi ya uchangiaji  wa shughuli za  Taasisi  ya Miracle Corners of the World ( MCW) hafla iliyokwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 15 tangu kuanziswa kwa  Taasisi hiyo  yenye  makazi yake Jijini New York, nchini Marekani.

Hafla hiyo  ilifanyika usiku wa Jumatatu na kuhudhuriwa na wageni wa kada  mbalimbali  yakiwamo makampuni makubwa  kama vile  NASDAQ OMX, CITI  na  the UPS Foundation ambayo yamekuwa yakichangia shughuli za  Taasisi  hiyo.  Miongoni mwa wageni waalikwa alikuwa ni  Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi
MCW  ilianzishwa mwaka 1999 na  Bw. Eddie  Bergman ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka kumi na  mitano, inajihusisha  miradi ya kijamii  ikiwamo ya huduma za afya, na uwezeshaji wa vijana na kukuza ushirikiano na  Taasisi nyingine.
Taasisi  hii  ilianza shughuli zake kwa kuanzisha kituo cha  vijana  jijini Arusha na baadaye  ikasambaza  huduma zake katika mikoa ya Iringa,  Dar es   Salaam, Ruvuma na Zanzibar.
“ MCW inajivunia  ushirikiano  na uhusiano wa karibu na Rais wa   Tanzania Mhe. Rais Jakaya Kikwete,  ambaye muwakilishi wake Balozi Manongi  yupo   pamoja nasi usiku huu. Ni ushirikiano na msaada wake wa hali na mali ndio  unaoifanya  MCW  iendele kutoa huduma zake nchini Tanzania. Napenda kutumia  fursa hii kumshukuru sana  Rais Kikwete”. Akasema Bw.
Katika miaka  yake  15 ya  shughuli zake  hususani uwezeshwaji wa vijana  kutambua vipaji vyao vya uongozi na kubwa zaidi uimarishaji  na uboreshaji wa huduma ya afya hususani afya ya  kinywa.  MCW imekuwa ikishirikiana   kwa karibu sana na Chuo  Kikuu cha Tiba na Sayasi  (MUHAS) katika  kuimarisha na  kuboresha Kitivo  cha Meno  kwa maana ya vifaa ,  mafunzo  na miundo mbinu.
 Ni katika hafla hiyo, ambapo  Rais na Mwanzilishi wa  MCW, Bw.  Eddie  Bergman wakati akielezea mafanikio ya  Taasisi  hiyo   alieleza kwamba  kontena lililokuwa na vifaa vyenye thamani ya dola za kimarekani 500.000 lilikuwa limewasili jijini  Dar es Salaam  ambapo kwa ushirikiano kati ya  Wizara ya   Afya na Ustawi wa Jamii na Bohari  Kuu ya  Madawa, ( MSD) kontena hilo limeshatolewa  bandarini na kukabidhiwa Chuo Kuu cha MUHAS.
Dkt. Marion Bergman ambaye  ni Mkurugenzi wa  miradi ya Afya katika  MCW alishuhudia kuwasili kwa kontena  hilo na makabidhiano.
Wakati wa hafla hiyo ya  jumatatu jumla ya dola za kimarekani 950,000 zilichangwa  kwa madhumuni ya kufanikisha shughuli za  Taasisi hiyo ambayo sasa  inazihusisha pia  Zambia,  Rwanda na  Sierra Leone
Akizungumza  katika hafla hiyo,  Balozi Manongi,  alieleza kwamba Tanzania  imekuwa mmoja wa wanufaikaji wakubwa wa MCW  na kwamba  Tanzania itaendelea kuenzi  shughuli zake ambazo zimelenga katika kuinua na kuimarisha huduma za afya katika  maeneo ya pembezoni mwa Tanzania.
Baadhi ya  washiriki  waliopewa  fursa ya kuzungumza na ambao wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na MCW walieleza kwamba kwa  kuja kwao  Tanzania  na kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na wadau mbalimbali wakiwamo vijana na wataalamu wa afya,  si tu kwamba wao wametoa, lakini  uzoefu walioupata katika maeneo waliyokwenda  umewabadili  kifikra na kimtazamo na kwamba wapo tayari wakati wowote kurejea  tena Tanzania.

No comments: