Social Icons

Friday 4 April 2014

MUHIMU: MKUTANO WA WIZARA YA KAZI NA AJIRA KUHUSU TAARIFA ZA UPOTOSHAJI

 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Kazi na Ajira Bw.  Ridhiwani Wema akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo piuchani) kuhusu taarifa za upotoshaji zinazotolewa na baadhi ya watu au makampuni binafsi kuhusiana na maudhui ya Tamko la Serikali lililoziagiza wakala binafsi  wa Huduma za Ajira  kuwasilisha upya maombi ya usajili wa uwakala kwa Kamishna wa Kazi.
 Afisa Kazi wa Wizara ya Kazi na Ajira Bw. Themistocles Rumboyo akiwaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuwa hadi kufikia Februari mwaka huu jumla ya maombi 56 ya makampuni ya huduma za ajira nchini yamewasilishwa kwa Kamishna wa Kazi. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bw. Ridhiwani Wema.
Afisa Kazi wa Wizara ya Kazi na Ajira Bw. Omari Sama akijibu swali la waandishi wa habari waliotaka kujua taratibu za kusajili wakala binafsi wa huduma za ajira hapa nchini. Kulia ni  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bw. Ridhiwani Wema. PICHA ZOTE NA FRANK MVUNGI- MAELEZO

No comments: