Thursday, 23 May 2013

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DODOMA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUGONGWA NA TRENI




Mwanafunzi  wa chuo kikuu cha Dodoma  anayejulikana  kwa jina  la Boid Mwakitalima  amefariki dunia  baada  kugongwa na treni....Mwanafunzi huyo  alikuwa  mwaka  wa  tatu.

Taarifa zinaeleza  kuwa, mwanafunzi  huyo  alikuwa   anatembea pembezoni  mwa  reli huku  akiwa ameweka  "headphone"  sikioni, hali  iliyomfanya  ashindwe  kusikia ama  kuhisi  chochote  juu  ya  muungurumo  wa  treni  hilo  mpaka  lilipomsogelea  karibu  na  kumsukuma  pembeni  ambapo  aliangukia  chuma  na  kuaga  dunia  pale  pale...
 Makamu Mkuu wa Chuo kikuu  cha Dodoma Prof.Idrisa Kikula  akiwasili Collage ya Informatics

 Mbele  ni Mshauri wa wanafunzi ( dean of student) chuo kikuu cha dodoma, Nyuma ni mshauri wa wanafunzi, Pro.Anatory  ( dean of students)  collage ya informatics na Katikati ni Makamu mkuu wa chuo cha Dodoma...
------ Baada  ya  ajali  hiyo, mwanafunzi  huyo  alipelekwa  chumba  cha kuhifadhia  maiti  katika  hospitali  ya  Mkoa  wa Domoma, "General hospital" ambapo  leo  hii  ameagwa  na wanafunzi wenzake  wa  chuo  kikuu  cha Dodoma  na  kusafirishwa  kwenda  nyumbani  kwao Mbeya kwa  mazishi..

 Wanafunzi wakiuaga  mwili  wa  marehemu  kwa  huzuni


 Mkuu wa  collage ya Informatics, Prof. Mvuma,  akitoa  nasaha  zake
 Rais  wa wanafunzi, collage ya informatics  akitoa  nasaha  zake


PICHA NA DJ SEK BLOG

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA" SIFURI KIBAO ZAFUTWA KIMYA KIMYA



MPANGILIO wa alama mpya za kufaulu kwa wahitimu wa kidato cha sita waliohitimu mwaka jana, ambao matokeo ya mitihani yao yanaweza kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa, unadaiwa kuzua aibu na kama si uamuzi uliotajwa bungeni wa matumizi ya alama za ufaulu za zamani, matokeo hayo yangeibua aibu kama ilivyojitokeza kwa kidato cha nne, 2012.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) ambalo linaendelea kupanga matokeo hayo ya kidato cha sita kwa kuzingatia alama za zamani kama ambavyo taarifa ya awali ya Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ilivyosomwa bungeni hivi karibuni, hali ingekuwa mbaya zaidi katika ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha sita kiasi cha kuweza kutishia uhai wa vyuo vikuu nchini kukosa wanafunzi wa kutosha.
“Hali ilikuwa mbaya sana kama alama za kufaulu zingeachwa zitumike zile mpya na si za zamani. Vyuo vikuu nchini visingeweza kupata wanafunzi wa kutosha.
 "Tatizo hapa si uwezo wa wanafunzi moja kwa moja katika kumudu mitihani bali ni kufanywa kwa mabadiliko ya alama bila kuwaandaa.
" Alama hizi zilipaswa kuanza kutumika na wanafunzi wapya, yaani kama wanaanza kidato cha kwanza wawe wanapewa mitihani ya kupimwa kwa kuzingatia alama mpya na waendelee nazo hadi mitihano yao ya mwisho.
“Na hivyo hivyo kwa wanafunzi wa kidato cha sita. Alama hizi mpya zinapaswa kutumika kwako kuanzia wakiwa kidato cha tano mara wanapoanza shule, kila mitihani wanayopewa isahihishwe na kupangiwa alama kwa kutumia hizi alama mpya,” kinaeleza chanzo chetu cha habari kutoka NECTA.
Kwa mujibu wa mabadiliko hayo ya alama, alama mpya zilizokuwa zimetumika awali ni daraja F kuanzia 34 hadi sifuri; badala ya alama hiyo F kuanzia 20 hadi 0; daraja D kwa kuzingatia alama mpya linapaswa kuanzia 35 tofauti na awali, yaani alama 21.
Taarifa zaidi zinabainisha ya kuwa, kati ya sababu za kuchelewa kutangazwa kwa matokeo ya kidato cha sita tofauti na muda uliotarajiwa yaani mwanzoni mwa Mei, ni pamoja na upangaji upya matokeo hayo, ikiwa ni tofauti na ilivyokuwa kwa kidato cha nne ambapo matokeo yalitangazwa na kisha kufutwa ili kuyapanga upya kwa kutumia alama za zamani.
Lakini alipoulizwa kuhusu masuala hayo ndani ya NECTA, Ofisa Habari wa Taasisi hiyo nyeti nchini, John Nchimbi alisema; “Kwa sasa niseme tu kwamba mchakato wa kuandaa matokeo ya kidato cha sita unaendelea, siwezi kusema lini hasa utakamilika lakini nina uhakika ni katika muda muafaka.”
Kuhusu matokeo ya kidato cha sita kucheleweshwa kutokana kupangwa upya ili kupunguza idadi ya waliofeli kutokana na matumizi ya alama mpya za kufaulu, Nchimbi anasema; “Unajua haya maagizo haya ya bungeni (kupanga matokeo kwa kuzingatia alama za zamani) yamekuja wakati mchakato wa kuandaa matokeo ulikwishaanza. Kwa hiyo baada ya maagizo ilibidi kufanya kazi hiyo tena kwa kufuata maagizo hayo.”
Hata hivyo, hakuweka bayana kama matokeo ya awali kabla ya maagizo ya Serikali yaliyotolewa bungeni kutumia alama za zamani yamewafanya wanafunzi wengi kufeli na badala yake akasema; “Hilo siwezi kulizungumzia kwa sababu mchakato wa matokeo hayo haukuwa umefika mwisho. Takwimu rasmi hazikuwa zimekamilishwa. Kwa hiyo si sahihi kusema rasmi walifeli.”
Lakini wakati hali ikiwa hivyo kwa upande wa matokeo yanayotarajiwa ya kidato cha sita, taarifa zaidi zinabainisha ya kuwa, baada agizo la serikali la kufuta na kurejewa upya kwa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012, takriban wanafunzi 50,000 wamepata unafuu katika matokeo yao tofauti na awali.
Awali, kwa kuzingatia matokeo ya kidato cha nne mwaka jana yaliyotangazwa Februari, mwaka huu jijini Dar es Salaam, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa, jumla ya watahiniwa 126,847 tu kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya mtihani huo walifaulu.
Katika matokeo hayo idadi ya wasichana waliofaulu ilitajwa kuwa ni 46,181 wakati wavulana waliofaulu ikiwa wanafunzi 80,686 na idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu ni 16,112 kati yao watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani wasichana ni 6,7751 na wavulana 9,361.
Katika matokeo hayo watahiniwa waliopata daraja la kwanza ni 1,641, daraja la pili 6,453 na daraja la tatu ni 15,426, wakati waliopata sifuri ni 240,903 lakini kwa kuzingatia taarifa za vyanzo vyetu ndani ya Baraza, idadi hiyo itabadilika kwa sababu ya alama kuongezwa kwa watahiniwa hao wa mwaka 2012.
Lakini matokeo hayo yalitangazwa pamoja na vituko walivyofanya baadhi ya wanafunzi, vikiwamo vituko vya kuandika matusi kwenye karatasi za majibu ya mitihani na kutokana na makosa hayo, watahiniwa 789 walifutiwa mitihiani yao.
Source: Raia Mwema.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA NANE YA KAMISHENI YA VYUO VIKUU MBALIMBALI JIJINI DAR ES SALAAM




  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, yatakayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yamefunguliwa leo. Picha zote na Muhidin Sufiani-OMR
Baadhi ya washiriki  wa maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akisoma hotuba yake ya kufungua rasmi maonyesho hayo ya siku tatu katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Maofisa wa mfuko wa PPF, kutoka (kushoto) ni Meneja wa Kanda ya Ilala, Evans Musiba, Meneja Uhusiano, Lulu Mengele na Ofisa Masoko, Sereki Michael, wakati alipotembelea katika banda la maonyesho la PPF, leo kwenye maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

PICHA NA OFISI YA MAKAM WA RAIS

Friday, 29 March 2013

MWANAFUNZI IFM AKUTWA AMEKUFA CHUMBANI







Mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha
(IFM), Ibrahim Jackson (24), amekutwa akiwa amekufa katika chumba cha
kupumzikia kilichopo chuoni hapo bila mwili wake kuwa na jeraha lolote. 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi, alisema tukio hilo lilitokea saa 11:30 juzi jioni katikachumba namba 118 jengo namba D kilichopo mtaa wa Shaban Robert. 
NIPASHE lilifika IFM na kuzungumza na
Mshauri wa Wanafunzi, Emmanuel Mushi, ambaye alisema kuwa marehemu
alikuwa anasomea Shahada ya Usimamizi wa Kodi akiwa mwaka wa pili. 
Alisema marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kifafa kwa muda mrefu kabla hata hajajiunga na IFM. 
Alisema juzi jioni marehemu aliomba
funguo kwa ajili ya kwenda kupumzika katika chumba kinachotumiwa kulala
na wanafunzi kutoka nje ya nchi pindi wanapofika chuoni hapo kwa ajili
ya masomo. 
“Nyaraka zake zinaonyesha marehemu
alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kifafa kwa muda mrefu, hata kabla
hajajiunga na chuo hiki, kwa hapa chuoni ugonjwa huo ulikuwa unamtokea
mara kwa mara,” alisema Mushi. 

Friday, 22 March 2013

MATOKEO YA RUFAA KIDATO CHA NNE 2012 AWAMU I YATANGAZWA TAZAMA HAPA



NECTA imetoa matokeo ya usahihishaji wa mtihani wa kidato cha nne Oktoba 2012  awamu ya kwanza kwa watahiniwa waliokata rufaa. 

Chanzo: Necta

Friday, 8 February 2013

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM SASA CHAPANDA JUU, KIPO KATIKA KUMI BORA YA VYUO VIKUU AFRIKA, TAZAMA HAPA!

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) sasa kinakamata nafasi ya sita katika Vyuo Vikuu 100 bora vya Afrika. Orodha kamili iko hapa Chini:2012 World University Ranking | Top 100 Universities in Africa
Source:http://www.4icu.org/topAfrica/

Top 100 Universities and Colleges in Africa by the 4icu.org University Web Ranking
1 University of Cape Town 
South Africa
2 University of South Africa 
South Africa
3 University of Pretoria 
South Africa
4 Universiteit Stellenbosch 
South Africa
5 University of the Witwatersrand 
South Africa
6 University of Dar es Salaam 
Tanzania
7 Cairo University 
Egypt
8 University of KwaZulu-Natal 
South Africa
9 The American University in Cairo 
Egypt
10 Makerere University 
Uganda
11 Rhodes University 
South Africa
12 University of the Western Cape 
South Africa
13 Mansoura University 
Egypt
14 University of Johannesburg 
South Africa
15 Université Cheikh Anta Diop 
Senegal
16 Assiut University 
Egypt
17 University of Nairobi 
Kenya
18 Zagazig University 
Egypt
19 University of Botswana 
Botswana
20 Université Mohammed V - Agdal 
Morocco

21 University of Ghana 
Ghana
22 Universiteit van die Vrystaat 
South Africa
23 University of Ibadan 
Nigeria
24 Addis Ababa University 
Ethiopia
25 North-West University 
South Africa
26 Alexandria University 
Egypt
27 Nelson Mandela Metropolitan University 
South Africa
28 University of Zambia 
Zambia
29 Université des Sciences et de la Technologie Houari Boumediène 
Algeria
30 The German University in Cairo 
Egypt
31 Obafemi Awolowo University 
Nigeria
32 Universidade Eduardo Mondlane 
Mozambique
33 University of Mauritius 
Mauritius
34 Ain Shams University 
Egypt
35 University of Lagos 
Nigeria
36 Tanta University 
Egypt
37 Université de Ouagadougou 
Burkina Faso
38 Kwame Nkrumah University of Science and Technology 
Ghana
39 Université de la Reunion 
Reunion
40 Université Nationale du Rwanda 
Rwanda
41 Helwan University 
Egypt
42 Cape Peninsula University of Technology 
South Africa
43 University of Zululand 
South Africa
44 Strathmore University 
Kenya
45 Université Cadi Ayyad 
Morocco
46 Al Akhawayn University 
Morocco
47 Université d'Alger 
Algeria
48 Université Mentouri de Constantine 
Algeria
49 Université Badji Mokhtar de Annaba 
Algeria
50 Université d'Oran 
Algeria
51 Université Hassan II - Casablanca 
Morocco
52 University of Fort Hare 
South Africa
53 Université Abdelmalek Essadi 
Morocco
54 Ahmadu Bello University 
Nigeria
55 Jaamacada Muqdisho 
Somalia
56 Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology 
Kenya
57 University of Swaziland 
Swaziland
58 University of Ilorin 
Nigeria
59 Sudan University of Science and Technology 
Sudan
60 Université Mohammed V - Souissi 
Morocco
61 Kenyatta University 
Kenya
62 University of Khartoum 
Sudan
63 University of Namibia 
Namibia
64 Université de Batna 
Algeria
65 University of Malawi 
Malawi
66 Benha University 
Egypt
67 Université Hassan II - Mohammedia 
Morocco
68 Al-Azhar University 
Egypt
69 Fayoum University 
Egypt
70 Université de la Manouba 
Tunisia
71 University of Benin 
Nigeria
72 Minoufiya University 
Egypt
73 Durban University of Technology 
South Africa
74 Université de Tunis El Manar 
Tunisia
75 Université de Carthage 
Tunisia
76 Tshwane University of Technology 
South Africa
77 United States International University 
Kenya
78 Université Abou Bekr Belkaid Tlemcen 
Algeria
79 Polytechnic of Namibia 
Namibia
80 Egerto University 
Kenya
81 Université de Gabès 
Tunisia
82 Université de Sousse 
Tunisia
83 Université d'Antananarivo 
Madagascar
84 Minia University 
Egypt
85 Moi University 
Kenya
86 Université de Nouakchott 
Mauritania
87 Université Mouloud Maameri de Tizi Ouzou 
Algeria
88 University of Venda 
South Africa
89 Central University of Technology 
South Africa
90 Université Ibn Tofail 
Morocco
91 University of Zimbabwe 
Zimbabwe
92 Suez Canal University 
Egypt
93 University of Cape Coast 
Ghana
94 Misr International University 
Egypt
95 University of Jos 
Nigeria
96 University of Maiduguri 
Nigeria
97 University of Limpopo 
South Africa
98 The Hubert Kairuki Memorial University 
Tanzania
99 Jimma University 
Ethiopia
100 Modern Sciences and Arts University

IMETOKA KWA SUFIANI MAFOTO BLOG

Thursday, 13 December 2012

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MGOGORO WA WAFANYAKAZI NA WANAFUNZI KATIKA CHUO KIKUU KISHIRIKI DAR ES SALAAM CHACHUO KIKUU CHA KIMATAIFA CHA KAMPALA



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 
TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA


Kwa takribani wiki tatu sasa kumekuwa na mvutano baina menejimenti kwa upande mmoja na wafanyakazi na wanafunzi kwa upande mwingine wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es salaam ama, kinavyojulikana kwa wengi, KIU. Mvutano huu ulisababisha baadhi ya waalimu kusitisha kufundisha na pia baadhi ya wanafunzi kujikuta katika mgomo hadi mvutano uliojitokeza utakapopatiwa ufumbuzi. 
Mvutano huu hatimaye ulisababisha Tume ya VyuoVikuu Tanzania kuingilia kati katika jitihada za kuupatia ufumbuzi. Mnamo tarehe 14 Novemba 2012 Tume iliunda timu ya wataalamu ambao walikwenda katika Chuo hicho na kufanya kazi kwa siku mbili kabla ya kuuanda ripoti yao. Ripoti ilibainisha maeneo mbalimbali yenye changamoto ambazo budi zipate majibu. 
Ripoti hiyo ilijadiliwa katika kikao cha Kamati ya Tume ya Ithibati na Chuo kupewa maelekezo katika maeneo mbalimbali na pia kutakiwa kuleta majibu katika masuala yaliyoonekana kuwa na uhitaji wa majibu. Maelekezo haya yaliwasilishwa Chuoni kwa barua ya tarehe 4 Desemba 2012 yenye kumbukumbu na TCU/A.40/69/Vol.IV/15 na kutakiwa kuleta majibu Tume kabla ya tarehe 30 Desemba 2012. Kabla majibu hayajawasilishwa mgogoro wa wafanyakazi ulianza na kufuatiwa na mgomo wa wanafunzi na hivyo tarehe 11 Desemba 2012 Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Elimu ya Juu walikwenda katika Chuo hicho ili kuonana hususan na wanafunzi pamoja na menejimenti. Kimsingi, kikao kilihusisha menejimenti na wanafunzi kwa kuwa suala la wafanyakazi lilikuwa limeshapatiwa muafaka wa jinsi ya kulitatua.
Kufuatia mawasiliano ya awali baina ya menejimenti ya Chuo na viongozi wa wafanyakazi kuhusu mishahara ya wafanyakazi ya mwezi wa Novemba 2012 pande zote zilikubaliana kwamba malipo hayo yawe yamefanyika ifikapo tarehe 14 Desemba 2012. 
Pia Chuo pamoja na waalimu wameafiki kufidia kipindi cha masomo ambacho kilipotea wakati wafanyakazi wanashughulikia mstakabali wa mishahara yao. Kufidia huko kutafanyika kati ya tarehe 7 Januari na 11 Februari 2013 ili kutokuathiri mipango mengine ya kimasomo ambayo tayari ilishapangwa kwa kipindi cha sasa hadi Januari 2013. Makubaliano haya yamewasilishwa TCU kwa barua ya Mkuu wa Chuo ya tarehe 10 Desemba 2012 yenye kumbukumbu Na. KIU/PR/Vol.30/11/12. Tume imeelekeza makubaliano haya yatekelezwe bila kukosa ifikapo tarehe 14 Desemba 2012. Ni matumaini ya Tume kwamba hali hii haitajitokeza tena ili shughuli za ufundishaji katika Chuo hicho ziende kulingana na ratiba ya kila semesta.
Kupata taarifa ya yaliyojiri katika kikao baina na menejimenti, wanafunzi, Katibu Mtendaji wa Tume na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Elimu ya Juu BOFYA HAPA.

Monday, 8 October 2012

SHEREHE ZA MAHAFALI YA 34 YA BODI YA TAIFA YA WAHASIBU NA WAKAGUZI WA HESABU


Mhitimu wa Shahada ya CPA ya  Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  ( NBAA)  , Gloria Joel Bendera , akipongezwa kwa kuoena mikono na Mgeni rasmi  Naibu Waziri wa Fedha , Janet Mbene  , baada ya kkumtunuku Shahada yake wakati wa Sherehe ya Mahafali ya 34 ya Bodi  hiyo yaliyofanyika Oktoba 6, 2012 kwenye viwanja vya Mhasibu , Barabara ya Biti Titi Momamed, Dar es Salaam.
 Baadhi ya wahitimu wa  mahafali ya 34 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  ( NBAA)  wakifurahia jambo wakati wa mazungunzo yao baada ya kutunikiwa Shahada ya CPA,  Oktoba 6, mwaka huu na Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha , Janet Mbene ( hayupo pichani)  katika  viwanja vya Mhasibu , Barabara ya Biti Titi Momamed, Dar es Salaam , Naibu Waziri huyo pia aliwatunukia wahitimu wengie vyeti .
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( kati kati ) na Mkewe mama Bendera akiwa katika  picha na mtoto wao,  Gloria Bendera , baada ya kutunikiwa Shahada ya CPA , Oktoba 6, 2012 wakati wa  mahafali ya 34 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  ( NBAA) ,Mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Waziri wa Fedha , Janet Mbene ( hayupo pichani) kwenye  viwanja vya Mhasibu , Barabara ya Biti Titi Momamed, Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( wapili kutoka kulia) akiwa  katika  picha na  baadhi ya wahitimu wa  mahafali ya 34 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  ( NBAA) wakiwa mtoto wake , Gloria Bendera ( watatu kulia mwenye mkoba mkononi)  baada ya kutunukiwa Shahada na Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha , Janet Mbene ( hayupo pichani)  Oktoba 6, 2012 katika  viwanja vya Mhasibu , Barabara ya Biti Titi Momamed, Dar es Salaam.
wadau wakifurahia Nondozzz zao. Picha zote na John Nditi wa Globu ya Jamii, Morogoro

Tuesday, 2 October 2012

Bodi ya Mikopo yasema imeshapeleka fedha vyuoni...!


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Profesa Idris Kikula


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imesema imeshapeleka fedha za chakula na malazi katika vyuo vyote vyenye sifa ya kupata huduma hiyo tangu wiki iliyopita.


Kauli hiyo ya HESLB, ilitolewa na Afisa Habari wake, Veneranda Malima, jijini Dar es Salaam jana.

Alisema kuhusu utaratibu wa wanafunzi kupata fedha hizo siyo jukumu la HESLB bali ni viongozi wa vyuo hivyo kwa utaratibu waliojipangia wenyewe.

Hata hivyo, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) cha jijini Dar es Salaam, kimesema fedha hizo hazijafika, lakini kimeahidiwa na HESLB kuwa zitapelekwa katikati ya wiki hii.

Waziri wa Mikopo wa Chuo hicho, Alek George, alisema:  “Sio kweli kwamba, fedha zimeshatumwa hapa chuoni, walituambia kuwa wiki hii watatupatia, lakini mpaka sasa bado.”

Wakati CBE wakisema hivyo, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kilisema kupitia kwa Kaimu Afisa wake wa Mikopo, Rajabu Kufiri, kuwa wameshasaini fedha hizo tangu wiki iliyopita na kwa sasa wako katika utaratibu wa kuwapatia wanafunzi fedha hizo.

Chuo cha Tumaini Kampasi ya Dar es Salaam kilisema bado hawajapewa fedha hizo kutokana na kuchelewa kufungua chuo, na kwa sasa utaratibu wa kuwasajili wanafunzi unaendelea ili kupata idadi kamili ya wanafunzi wanaoendelea na masomo.

Afisa Mikopo wa Chuo hicho, Ukende Mwakitwange, alisema juzi HESLB waliwapatia orodha ya wanafunzi waliosajiliwa katika chuo hicho, lakini fedha hawajapatiwa.

Makamu  Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Profesa Idris Kikula, alisema: “Bado hatujapata mikopo na leo hii (jana) nimetoka kuzungumza na wenzangu kuhusiana na suala hilo la mikopo kwa wanafunzi.”

Alisema kutokana na hali hiyo utawala umeamua kumtuma mtu kwa ajili ya kufuatilia suala hilo HESLB.

Afisa Habari wa Chuo Kikuu cha St. John, Karim Meshack, alisema HESLB imewapelekea majina ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza, ambao wanastahili kupata mikopo. 

Alisema mikopo hiyo inaweza kufika chuoni hapo mara baada ya wanafunzi hao kufanyiwa usajili. 

Naye Afisa Mikopo wa Chuo cha Mipango, Daud Nyagalu, alisema: “Bado hatujapata mikopo na tunaendelea kufuatilia.” 

Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara (MUCCoBS), Profesa Faustine Bee, alisema: “Tunatarajia kufungua chuo Oktoba 15, mwaka huu, wanafunzi watakapofika chuoni ndio tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuzungumzia kama wametuingizia fedha au la, matarajio yetu ni kupata fedha hizo kwa wakati.”

Uongozi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Stephano Moshi (Smmuco), ulisema chuo bado hakijafunguliwa na baada ya kufunguliwa ndio watakuwa kwenye nafasi nzuri ya kueleza juu ya fedha za wanafunzi hao kama zimeingizwa kwenye akaunti au la.

Chuo cha Ustawi wa Jamii hakipapata fedha hizo na habari kutoka ndani ya uongozi zinaeleza kuwa chuo kilichelewa kufanya mitihani na kupeleka majina katika Bodi.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kilisema fedha hizo zingepelekwa chuoni hapo Alhamisi iliyopita, jana kilishindwa kuthibitisha kuzipokea baada ya Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandara, kueleza kuwa alikuwa mbali na chuo.

Hata hivyo, Naibu Makamu Mkuu wa UDSM (Utawala), Profesa Yunus Mgaya na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Frolence Luoga, hawakupatikana.

Imeandikwa na Gwamaka Alipipi, Amos Mbungu na Issaya Kisimbilu, Dar; Jacqueline Massano, Dodoma; na Salome Kitomari, Moshi.
CHANZO: NIPASHE

Saturday, 22 September 2012

KILIO CHA WANAFUNZI WANAOJIUNGA NA CHUO KIKUU CHA DODOMA



 


Salaam,
tafadhali tusaidie sisi wanafunzi wa Mwaka wa kwanza tuliochaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambao hadi leo hatujapata Admission Letters zetu hadi hii leo na Baadhi tunatakiwa tuzitumie hizo kuombea ruhusa makazini hasa wafanyakazi wa Serikali, je tunafanyaje na UDOM waliweka tangazo hili hapa chini wiki ya ya pili na zaidi sasa.

Tunashangaa barua hazitoki ilhali TCU wao wamesha toa majina ya watakao jiunga hapo na hata Bodi ya Mikopo nayo imetoa majina.

Tunaomba tupatiwe barua zetu maana Chuo karibia kinafunguliwa kwa sisi wa 1styear.

Admission Letters For First Year Students for Academic Year 2012/2013

Announcement to All first year Students for Acadmic Year 2012/2013
Be Informed that If your Name Do not appear on the List of Selected Students Published on UDOM website, you will not be able to Download your Admission Letter. For Second batch and Equivalent Students the list of Selected Students will be publised at Mid the Next Week.
For those who their Names Appears on the List, The admission Letters are Downloaded on the following Link, Please make sure you Read the Instructions.

NAWASILISHA


Friday, 21 September 2012

HAYA NDIYO MAJINA YA WANAFUNZI WALIO CHAGULIWA KUJIUNGA NA ELIMU YA JUU 2012/2013, PIA TAZAMA MAJINA YA WALIO PATA MKOPO PAMOJA NA SCHOLARSHIPS HUKO MOZAMBIQUE !


SELECTED APPLICANTS FOR THE 2012/2013 ADMISSIONS

The Tanzania Commission for Universities (TCU) in Collaboration with the National Council for Technical Education (NACTE) is announcing the names of Applicants who were seleted into various programs for the 2012/2013 Admissions. However, the list of  some applicants who were selected into various programs but obtained no loan, applicants who were returned by some institutions, and selected applicants who asked for transfer, will be announced before 21 September 2012
 
To view selected applicants with Loans, please click here...

To view selected applicants through Mozambique Scholarships, please click here...

To view selected applicants with Loans but subject to verification with HESLB (Previous Lonee), please click here ... 
 

WANAFUNZI WALIOPATA MIKOPO 2012/2013 BOFYA HAPA

KWA MAELEZO ZAIDI INGIA http://www.tcu.go.tz

Monday, 17 September 2012

Wasiwasi wa mikopo wakumba wanafunzi vyuo vikuu





Wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini, wako hatarini kuchelewa kupata fedha za mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kutokana na mchakato wa kutoa mikopo hiyo kuchelewa kuanza.

Hali hiyo inatokana na vyuo hivyo kuanza kufunguliwa mwishoni mwa mwezi huu na mwanzoni mwa mwezi ujao.

 Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE umebaini kuwa wanafunzi katika vyuo hivyo walioomba mikopo toka HESLB, bado hawajaanza kupata hatua ambayo imeanza kuwapa shaka kama wataripoti vyuoni kwa wakati kutokana na kutegemea fedha za mikopo kwa ajili ya ada ya masomo na mahitaji mengine.

Kutokana na ucheleweshaji wa mikopo hiyo, gazeti hili lilishudia wanafunzi kadhaa ambao wamedahiliwa kujiunga vyuo vya elimu ya juu mwaka huu, wakimiminika katika ofisi za HESLB makao makuu jijini Dar es Salaam kuulizia hatma ya mikopo waliyoomba.

“Unavyoniona hapa ni wiki ya tatu nimekuwa nikija hapa ofisi za Bodi ya Mikopo kuulizia kama mikopo imeanza kutolewa, lakini tunaelezwa tuendelee kusubiri wakati vyuo vimekaribia kufunguliwa,” alisema mwanafunzi mmoja aliyetoka Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro.

Hata hivyo, Afisa mmoja wa HESLB, aliyejitambulisha kwa jina moja la Venelanda, alisema mchakato wa kuandaa mikopo ya wanafunzi bado unaendelea na kwamba zoezi hilo linachukua muda kidogo kutokana na mikopo hadi kukamilika kwake hupitia maeneo mengi.

Venelanda ambaye hata hivyo, hakutoa jibu la moja kwa moja kama mikopo kwa wanafunzi hao itaanza kutolewa lini, alisema HESLB itahakikisha mikopo hiyo inatolewa kwa wanafunzi hao kabla ya kufunguliwa vyuo hivyo.

Mkuu wa Idara ya Habari Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, alipoulizwa na gazeti hili kama fedha za mikopo kwa wanafunzi wa  elimu ya juu zimeshapelekwa HESLB, alisema suala hilo waulizwe Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

“Bajeti ikishapitishwa bungeni, kinachobakia ni kwa wizara husika kushughulikia mipango yake, hivyo hata suala la fedha za mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu  wenye majibu ni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,” alisema Mduma.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillipo Mulugo, alipoulizwa na NIPASHE, alisema kimsingi mikopo bado haijaanza kutolewa kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu na kufafanua kuwa kuanzia wiki hii wizara yake itaangalia uwezekano wa kushughulikia suala hilo ili wahusika wapewe mikopo hiyo.

Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), Bhokombe Itembe, alisema wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanatarajia kuripoti chuoni hapo Oktoba Mosi, mwaka huu.

Alisema wiki iliyopita uongozi wa chuo na Daruso, walitaka kupanga vyumba katika hosteli kwa ajili ya wanafunzi, lakini zoezi hilo lilishindikana kwa sababu bado haijafahamika idadi ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza watakaoripoti chuoni hapo.

Itembe alisema tatizo la kuchelewa kwa mikopo linatokana na sababu kadhaa, ikiwemo kutokuwepo kwa ushirikiano kati ya HESLB na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).

“Mwanafunzi anapodahiliwa bila TCU kumuamulia ataenda chuo gani, huwezi kwenda na wakati huo huo bila HESLB kukupatia mkopo, vile vile huwezi kwenda chuoni,” alisema Itembe.

Rais wa Chuo Kikuu cha Usimamizi wa Fedha IFM, Michael Chazy, alisema chuo hicho kitafunguliwa Oktoba 8, mwaka huu na kwamba hadi sasa bado wanafunzi wanaoendelea na wale wa mwaka wa kwanza hawajaanza kupatiwa mikopo.

Naye Rais wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Paul Yunge, alisema suala la mikopo katika chuo lina utata hasa kwa wanafunzi wanaoanza mwaka wa kwanza ambapo baadhi yao wamejaza fomu vibaya na hivyo taasisi husika zinashughulikia tatizo hilo.

Rais wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Amos Chakushemeire, alisema utoaji wa mikopo hauridhishi kabisa katika chuo hicho ambapo wanafunzi walioanza muhula Julai, mwaka huu, wamelipwa robo ya mkopo wakati kiasi kingine cha mkopo hawajalipwa hadi sasa, hali ambayo imesababisha ukata mkubwa kwa wanafunzi.

“Chuo chetu ni tofauti na vingine, kina mihula mitatu, wanafunzi walioanza muhula wa Julai hawajalipwa sehemu nyingine,. Hivi karibuni uongozi wa chuo ulilazimika kuwakopesha Sh. 50,000 wanachuo hao ili kuwatuliza wasigome,” alisema Chakushemeire.

Rais wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Frank Nkinda, alisema mikopo ni changamoto kubwa katika chuo hicho ambapo wanafunzi wa mwaka wa kwanza hawajapata mikopo hadi sasa.

Alisema kutokana na hali hiyo, hivi karibu Mwenyekiti wa HESLB alifika chuoni hapo kuzungumza na uongozi, serikali ya wanafunzi na wanachuo ambapo alitoa ahadi kutoa mikopo kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika mwaka huu wa 2012/2013.

Mwaka jana serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilitangaza utaratibu mpya wa utoaji wa mikopo ambapo badala ya fedha hizo kutolewa kwa waombaji na HESLB, sasa fedha hizo zinapelekwa vyuoni ambako menejimenti za vyuo zinawajibika kuzisimamia na kuwapa waombaji.

Hatua hiyo ilifikiwa ili kurahisisha mchakato wa kuwapatia fedha waombaji na pia kuepusha usumbufu kwa HESLB kutokana na wanafunzi kutoka vyuoni kuvamia ofisi hizo kwa lengo la kushinikiza wapewe fedha.

Taarifa iliyotolewa na HESLB na TCU Agosti 10 na 12, mwaka huu ilieleza kuwa zaidi ya wanafunzi 3,074 walioomba mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka 2012/13, wameenguliwa katika maombi yao kutokana na dosari mbalimbali.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa HESLB pekee iliorodhesha zaidi ya wanafunzi 2,649 ambao ilibaini kuwa na mapungufu kadhaa katika maombi yao ya kupewa mikopo.

Miongoni mwa makosa ama dosari ambazo HESLB ilizibaini kwa walioenguliwa ni pamoja na kukosekana kwa vyeti vya kuzaliwa kwa muombaji, sahihi ya mdhamini/muombaji, kukosekana kwa picha ndogo ya muombaji/mdhamini, kukosekana kwa sahihi za viongozi wa serikali za mitaa/vijiji kwa waombaji na nyaraka nyingine muhimu kwa waombaji.

Kwa upande wake TCU, iliwaengua jumla ya waombaji 425 kwa dosari na makosa mbalimbali.

Miongoni mwa dosari ambazo zilitajwa na TCU ni pamoja na baadhi yao kukosea namba za vyeti vya masomo kwa vidato vya nne na tano, miaka ya kumaliza masomo, mawasiliano sahihi kwa muombaji pamoja na uchaguzi wa masomo.

Hata hivyo, taasisi hizo mbili zimetoa muda kwa walioenguliwa sasa kutokana na dosari hizo kurekebisha na kutuma tena maombi yao kupitia mitandao kwa mujibu wa maelekezo waliyotoa.

Kwa mwaka huu wa fedha 2012/13, serikali imeiongezea fedha HESLB kwa kuitengea Sh. bilioni 326 kwa wanafunzi 98,772.

Mwaka jana, serikali iliitengea HESLB Sh. 91,722,783,264  kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Ucheleweshaji wa fedha za mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu umekuwa ukisababisha wafanye migomo, vurugu na maandamano mara kwa mara kushinikiza walipwe.




 NA THOBIAS MWANAKATWE
CHANZO: NIPASHE