Social Icons

Featured Posts

Tuesday 17 April 2018

UNDP YASAIDIA TANZANIA KUKUSANYA TAARIFA ZA HALI YA HEWA YA UKAA

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

Na: Calvin Edward Gwabara.


Shirika la maendeleo la umoja wa mataifa UNDP linaisaidia Tanzania kuwa na mfumo bora wa kukusanya na kuhifadhi taarifa za hewa ya ukaa nchini ili taarifa hizo ziweze kutumika katika mipango mbalimbali ya kusaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kuwa na taarifa sahihi za mchango wan chi katika kukabiliana na tatizo hilo.
Baadhi ya washiriki mafunzo hayo kutoka wizara mbalimbali na vyuo vikuu wakifuatilia mafunzo ya namna ya kutumia mfumo huo.
Akizungumza na Waandishi wa habari wakati wa mafunzo kwa wadau wakuu wa mpango huo na namna ya kutumia mfumo huo katika kukusanya taarifa hizo mtaalamu wa miradi inayohusu nishati na mabadiliko ya tabia nchi kutoka UNDP tawi la Tanzania Bwana Abbas Kitogo amesema mfumo huo utaiwezesha Tanzania kuwa na takwimu sahihi za hali ya hewa ya ukaa na namna tunavyopambana katika kuipunguza .
Ameongeza kuwa kwa sasa Tanzania hatuna taarifa sahihi na rasmi sana pale inapotakiwa kueleza mchango wetu kama taifa katika kutatua changamoto hiyo na hivyo kushindwa kujua kama nchi tufanye tuongeze nguvu wapi au tufanye nini katika kusaidia jitihada hizo za dunia.

Friday 2 February 2018

KAIMU KATIBU IDARA YA VYUO,VYUO VIKUU AKABIDHI KADI 1500 KWA KATIBU HAMASA SENETI YA DAR

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
Kaimu Katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu Ndugu Daniel Zenda akikabidhi  kadi 1500 za wanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kwa Katibu wa Hamasa Seneti ya mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Juakali Kuwanya katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya UVCCM, Upanga  jijini Dar es Salaam.

Zenda amesema, kadi hizo amezikabidhi ili zigawiwe kwa wananchama wapya ambao wamekuwa wakijiunga kwa wingi katika Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake, kutokana na mwamko mkubwa wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuunga mkono CCM kutokana na kuvutiwa na Utendaji kazi  wa Rais John Magufuli na Serikali yake ya awamu ya tano

Imetolewa na 
Uvccm Seneti Mkoa Dsm.

Tuesday 30 January 2018

MPYA KABISA TAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2017 HAPA

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 
 CHANZO NECTA

Thursday 25 January 2018

Mwanafunzi SUA asakwa kwa tuhuma za kumnyonga mpenzi wake

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
 Jeshi la polisi mkoani Morogoro linamsaka mwanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Mwita Marwa (30) kwa tuhuma za kumuua kwa kumnyonga mpenzi wake Kibua Adam (39) baada ya kutokea kutokuelewana kati yao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amesema tukio hilo lilitokea Januari 22 mwaka huu katika eneo la Modeco Manispaa ya Morogoro ambapo mwanafunzi huyo alitoweka baada ya tukio hilo.

Amesema siku ya tukio mwanafunzi huyo na mpenzi wake ambaye ni mhudumu wa baa walichukua chumba katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kama Aluta ambapo walilala lakini baadaye mwili wa marehemu ulikutwa chumbani.

“Dada huyu mkazi wa Kihonda alikutwa ameachwa chumbani akiwa ameshafariki na baada ya uchunguzi ilionekana kwamba marehemu alinyongwa shingo kabla ya kifo chake,” amesema Kamanda Matei.

Hata hivyo, kamanda huyo amesema baada ya tukio hilo mtuhumiwa alimwandikia ujumbe wa simu dada wa marehemu aitwaye Happiness Adamu ujumbe akisema kwamba tayari marehemu keshatangulia na yeye mtuhumiwa atafuata.


“Nasikitika sana hamtatuona hapa duniani Mwita na Kibua, mimi ninayeandika meseji hii ni Mwita, nikimaliza nakunywa sumu au vidonge nife na mimi nimechoka na dunia na Kibua yeye keshatangulia, njooni hapa Aluta Bar mtutoe chumbani tulipolala,” ulisomeka ujumbe huo.

Hata hivyo, watu wa karibu wa marehemu ambao hawakutaka kutaja majina yao walisema marehemu alikuwa na mpenzi mwingine kabla ya Mwita na walipokorofishana ndipo alipoamua kuwa na Mwita lakini siku chache kabla ya tukio alimwambia Mwita kwamba mpenzi wake wa awali amejirekebisha hivyo anataka kurejeana naye jambo ambalo mtuhumiwa alikuwa analipinga.

Kamanda Matei amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa ya Morogoro na jeshi hilo bado linaendelea na jitihada za kumsaka mtuhumiwa.   

Wednesday 24 January 2018

NAIBU WAZIRI WA ELIMU ATAKA VIFAA VYENYE THAMANI YA SH 14 BILIONI VIFUNGWE HARAKA

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.

Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,William Ole Nasha akitoa hotuba yake wakati wa mahafali ya tisa ya Chuo cha Ufundi Arusha(ATC) 
Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,William Ole Nasha(wa pili kuli) akiwapongeza wanafunzi wahitimu waliofanya vizuri zaidi katika kozi walizosomea 
Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,William Ole Nasha(katikati),Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha(ATC),Dk Masudi Senzia(wa pili kulia),Makamu Mkuu wa Chuo,Utawala,Fedha na Mipango,Dk Erick Mgaya pamoja na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wasichana. 


Arusha.Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,William Ole Nasha ameuagiza uongozi wa Chuo cha Ufundi Arusha(ATC) uwe umefunga vifaa vya kisasa vyenye thamani ya Sh 14 bilioni ndani ya wiki nne badala ya siku 67 ili vianze kutumika mara moja.

Ametoa agizo hilo kwenye mahafali ya tisa ya wahitimu 465 wa fani mbalimbali za ufundi jijini hapa kuwa ukarabati na upanuzi wa karakana ufanyike ndani ya muda alioutoa ili vifaa hivyo vitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

"Nilipotembelea Chuo hiki Desemba 2,mwaka jana nilitoa maagizo mharakishe ujenzi na ukarabati wa miundombinu itakayotumika kufunga vifaa hivyo kutoka Austria,nafarijika kusikia kuwa utaanza mara moja kwani Wizara ilishatoa kibali cha kutumia watalaam wenu wa ndani na fedha mnayo,"alisema Ole Nasha

Alisema sekta ya elimu ya ufundi kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2015 inatarajiwa kuleta maendeleo ya haraka ya rasilimali watu walioelimika na kupenda kujielimisha zaidi ili kulifanya taifa lipate maendeleo.Ole Nasha aliongeza kuwa elimu ya ufundi ina mchango mkubwa katika kufikia uchumi wa kati unaotegemea viwanda na nchi zilizoendelea kama Japan na China zimefikia hapo zilipo kwa kutilia mkazo elimu ya ufundi.

"Katika Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo 2016/17 hadi 2020/21 tunalenga kuongeza idadi ya wahitimu wa Vyuo vya Ufundi Stadi(Veta) kutoka 150,000 hadi 700,000 na Vyuo vya Elimu ya Ufundi vinavyotoa elimu ya Kati kutoka 40,000 hadi 80,000,"alisema 

Kuhusu idadi ya wasichana wanaosoma elimu ya ufundi kuwa ndogo alivitaka vyuo vyote vya ufundi nchini kuweka mikakati ya kuongeza udahili ikiwa ni pamoja na kutoa kipaumbele maalum kwa kwa wanafunzi wa kike wanaomba kujiunga.

Pia aliagiza Mamlaka ya Elimu nchini(TEA)kuharakisha upatikanaji wa fedha kiasi cha Sh 1.7 bilioni kilichotengwa kwaajili ya ujenzi wa hosteli za wasichana katika Chuo hicho ili kupunguza pengo katika wavulana na wasichana.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha ATC,Dk Masudi Senzia alisema wahitimu 465 wamemaliza katika ngazi za Astashahada ya awali,Astashahada ,Stashahada na Shahada huku wahitimu wa kike ni 101 sawa na silimia 21 na wahitimu wa kiume ni 364 sawa na asilimia 78.

Wednesday 3 January 2018

MAELEKEZO YA BODI YA MIKOPO KWA WADAIWA AMBAO BADO HAWAJAAJIRIWA

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imewataka wanufaika wote wa mikopo ambao wanadaiwa na hawajaajiriwa bado, wafike katika ofisi za bodi hiyo zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini ama kuwasiliana nao, ili wapewe maelekezo na utaratibu maalum wa namna ya kulipa mikopo yao.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Bodi ya Mikopo zilizoko Mwenge, Jijini Dar es Salaam, mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa elimu ya Juu (HESLB), Abdul-Razaq Badru ametoa wito kwa wale ambao bado hawajaanza kurejesha mikopo yao, hata kama bado hawajapata ajira maalumu, wafike katika ofisi za bodi maeneo mbalimbali nchini ili kupewa maelekezo na utaratibu wa namna ya kuanza kurejesja mikopo hiyo.

“Tunatoa wito kwa wale ambao kwa sababu fulani fulani walikuwa hawajaanza kulipa, walipe na wanakaribishwa kwenye ofisi zetu. Hata wale ambao hawako kwenye ajira maalum kuna utaratibu maalum tumewatengenezea. Wanaweza kuwasiliana na sisi katika mawasiliano yetu au wakaja ktika ofisi za Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha, Zanzibar na kwingineko il tuwape maelekezo na utaratibu maalum wa kulipa.” amesema Mkurugenzi Badru

Aidha Mkurugenzi Badru amesisitiza kuwa Bodi itahakikisha kuwa inawashughulikia wale wote ambao bado hawajarejesha mikopo yao ili waweze kuirejesha ikiwemo kuwachukulia hatua za kisheria na kuwafikisha mahakamani.

“Mtu yeyote aliyekopa mkopo kwa ajili ya kusoma, njia pekee ya kisheria inayoweza kumfanya asilipe mkopo huu, ni labda awe amefariki. Lakini kama umekopa, uko hai, uko hapa nchini na hata ukienda nje, sisi ni lazima utalipa huo mkopo kwa gharama yoyote ile,” amesisitiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Urejeshaji wa Mikopo, Phidelis Joseph amewataka wale ambao tayari wameshaanza kurejesha madeni katika akaunti za benki za Bodi ya Mikopo, waweke maelezo yote katika ”pay-in-slip’ zao.

“Wale wanufaika ambao wanajitokeza na wanalipa kwenye zile ‘bank accounts’ zetu waweke ‘details’ zote. ‘Unapodeposit’ unatakiwa utoe taarifa kwa Bodi ya Mikopo kwamba nimeweka pesa. Lakini vie vile unapoiandika ile ‘slip’ yako uiandike vizuri..,” amesema Phidelis Joseph.

Vile vile amewataka wanufaika wa mikopo ambao wameshaanza kulipa, wafike katika ofisi za Bodi ya mikopo ama kutumia mitandao ya Bodi, kwaajili ya uhakiki.

BODI YA MIKOPO (HESLB) YAWAGEUKIA WAAJIRI

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (HESLB) imesema kuanzia Jumatatu ijayo, Januari 8, 2018 itaanza kukagua taarifa za mishahara za waajiri (payroll) ili kubaini waajiri ambao wanawasilisha kiwango kidogo cha mikopo ya wafanyakazi wao ambao ni wanufaika pamoja na waajiri ambao hawawasilishi kabisa pesa hizo kwenye bodi hiyo kwa mujibu wa sheria ili wachukuliwe hatua stahiki.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru amesema wanufaika wengi wa mikopo, wakiwemo wadaiwa sugu, wameonesha ushirikiano mkubwa katika kurejesha mikopo yao, hivyo kurahisisha kazi ya kukusanya madeni ya mikopo hiyo.

“Kiasi cha pesa za wadaiwa sugu kilichoiva na kinachotakiwa kuwasilishwa ni Tsh. bilioni 285, hii inajumuisha kuanzia kazi hii ya kukopesha ilipoanza.

“Tangu mwaka jana mpaka sasa tumewapata wadaiwa sugu 26,000, tunashukuru wanufaika hawa wamejitokeza na wanawasilisha mikopo yao. Kuna baadhi ya waajiri wanawasilisha vizuri marejesho ya wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu, wengine hawasilishi na wengine wanawasilisha kiasi kidogo tofauti na asilimia 15 kama sheria inavyotamka.

“Kuanzia Jumatatu, Jan. 8, 2017 tutaanza kukagua taarifa kwenye payroll za waajiri wote waliosajiriwa kubaini waajiriwa wao ambao ni wanufaika wa mikopo wanaodaiwa ili waweze kukatwa.

“Lengo la kufanya ukaguzi kwenye payroll za waajiri ni kubaini iwapo wana waajiriwa wanadaiwa na HESLB, waajiri wanaowasilisha kiwango kinachotakiwa, wanaowasilisha chini ya asilimia 15 na wanaokata pesa na hawaziwasilishi HESLB,” alisema Badru.

Hata hivyo, Badru amesema wamelazimika kufungua ofisi zao nchi nzima kwa ajili kusimamia malipo ya fedha hizo za mikopo, hasa wale waliotajwa kwenye orodha ya wadaiwa sugu ambapo wamewasambaza wakaguzi nchi nzima, kwa ajili ya kufuatilia waajiri wasiotekeleza wajibu wao wa kuwakata asilimia 15 wanufaika hao waliowaajiri.

Monday 4 December 2017

WAZIRI KIJAJI AWATAKA WAHITIMU CHUO CHA UHASIBU ARUSHA KUJIEPUSHA NA RUSHWA

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji ambaye alikuwa mgeni rasmi akizungumza juzi katika mahafali ya Chuo cha Uhasibu Njiro Arusha ambapo pamoja na mambo mengine amewaonya wahitimu nchini kujiepusha na rushwa kwa kutaka utajiri wa haraka kuacha tabia hiyo kwani hawatabaki salama katika utawala huu. (Habari Picha na Pamela Mollel,Arusha)
 Mwenyekiti wa Bodi ya chuo cha uhasibu Arusha Bi.Rukia Adam akisoma maelezo ya chuo cha Uhasibu Arusha katika mahafali chuoni hapo juzi

Mkuu wa kitivo cha uhandisi,mazingira na Computer Paul David Greening kutoka Uingereza akizungumza katika mahafali yao juzi katika Chuo cha Uhasibu NjiroArusha
Kushoto ni mgeni rasmi ambaye ni NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji akisoma maelezo mafupi ya chuo cha Uhasibu Njiro Arusha katika mahafli juzi chuoni hapo


 Wahitimu wakifatilia mahafali hayo kwa ukaribu zaidi
 Meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja,wapili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Njiro,Dk.Faraji Kasidi akiteta jambo Naibu  Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji katika mahafali chuoni hapo juzi


Wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika masomo yao wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi

Baadhi ya watumishi wa chuo hicho wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi juzi katika mahafali chuni hapo

Na Pamela Mollel,ARUSHA 
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji ametoa onyo kali kwa  wahitimu wa Uhasibu nchini kujiepusha na rushwa kwa kutaka utajiri wa haraka kuacha tabia hiyo kwani hawatabaki salama katika utawala huu. 

Akizungumza juzi  katika mahafali ya 19 katika Chuo cha Uhasibu Njiro Arusha, wakati akitunuku vyeti vya ngazi mbalimbali viiwemo vya Uhasibu kwa wahitimu 1324, Dk.Ashatu alisema baadhi ya wataalamu wa Uhasibu wanachangia kurudisha nyuma Maendeleo kwa tamaa zao.

Alisema ni vema watumie elimu waliopata kubuni ajira na pale watakaotoa ajira wafanye kwa weledi na uadilifu.

Alisema endapo wataalamu hao watabadilika na kuwa na uadilifu itawezesha Taifa kufanikisha ndoto yake ya kufikisha uchumi wa Viwanda kabla ya mwaka 2025.

Aidha alipongeza Chuo kuwa wabunifu wa kuongeza kozi kulingana na huhitaji wa jamii hadi kufikia 33 ikiwemo ya Shahada mpya ya Kijeshi ilioanza kutolewa mwaka huu.

Kuhusu ombi la ujenzi wa Hosteli na kumbi za Mihadhara, alisema serikali itazitatua kulingana na jinsi wanapopata fedha,japo alishauri uongozi wa Chuo kuhakikisha sekta  binafsi wanaona watawasaidiaje.

Naye Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Njiro,Dk.Faraji Kasidi alisema mwaka huu wameadhimisha  Mahafali  ya 19 ya Chuo hicho na ya nane ya Chuo hicho Kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Coventry ya Uingereza.

Alishukuru serikali kwa kutoa mikopo kwa nusu ya wanachuo wa mwaka wa kwanza 2017 na kufanikisha ndoto kwa watoto maskini.

Mwisho

Tuesday 21 November 2017

NGONGAMANO LA WASOMI WANATAALUMA KUFANYIKA JUMAMOSI HOTELI YA LANDMARK UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

 Mratibu wa Kongamamo la Wasomi Wanataaluma wa Kikristo liitwalo Tanzania for Jesus Prayer Movement ambalo mlezi wake ni Huduma ya I Go Africa for Jesus,  Ephrahim Mwambapa akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Kanisa la Abundant Bressing Center (ABC), Tabata Matumbi jijini Dar es Salaam, kuhusu kongamano hilo litakalofanyika Hoteli ya Landmark siku ya Jumamosi. Kulia ni Mjumbe wa Kongamano hilo, Lendian Bigoli.

Mratibu wa Kongamano hilo, Ephrahim Mwambapa akisisitiza jambo kwenye mkutano huo. Kushoto ni Kiongzi Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Center nchini, Askofu Flaston Ndabila.

Na Dotto Mwaibale

WANAFUNZI waliohitimu vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini Jumamosi ya Wiki hii wanatarajia kufanya kongamono kubwa la kihistoria kujadili namna watakavyoweza kutumia taaluma zao kusaidia jamii, kanisa na taifa kwa ujumla.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Mratibu wa Kongamamo hilo, Ephrahim Mwambapa alisema kongamanao hilo linaundwa na muungano wa wasomi wa kristo uitwao Tanzania for Jesus Prayer Movement ambao mlezi wake ni Huduma ya I Go Africa for Jesus.

Alisema licha ya muungano huo kuundwa na vijana wa kikristo lakini vijana wote wasomi kutoka katika vyuo na shule za sekondari na madhehebu mbalimbali wanaalikwa ili kuchangia mada zitakazo jadiliwa na mgeni rasmi atakuwa ni Kiongzi Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Center nchini, Askofu Flaston Ndabila.

Mwambapa alisema kuwa katika kongamano hilo kutakuwepo na mada mbalimbali na kuona ni jinsi gani kila mmoja na taaluma yake ataweza kusaidia jamii badala ya taaluma hiyo kuachwa bila ya kuifanyia kazi.

"Tunapokuwa vyuoni tunakuwa na mipango mingi ya maendeleo lakini baada ya kumaliza masomo kila mtu anakuwa kivyake wakati tunapaswa kushirikiana na jamii na ndio maana tumeona ni vizurio kuazisha muungano huu lengo likiwa kujumuika na jamii katika shughuli za maendeleo ya nchi na dini" alisema Mwambapa.

Alisema wazo la kuanzisha muungano huo nimatunda ya mkutano ya mkutano mkuu wa kitaifa wa kuliombea taifa ulioratibiwa na Askofu Flaston Ndabila na kuhudhuriwa na watu mbalimbali na vijana kutoka vyuo vikuu uliofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mwambapa alisema kongamano hilo litafanyika Hoteli ya Landmark Ubungo jijini Dar es Salaam na litahudhuriwa na wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali,sekondari baadhi wa viongozi.

MWANAFUNZI WA CHUO CHA UHAZILI TABORA AKUTWA AMEJINYONGA KWA KUTUMIA TAI.

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
21 November 2017.
MWANACHUO mmoja Chuo cha Utumishi wa Umma –Tawi la Tabora kinachojulikana kama Uhazili  Raphael Kadesha (22)  amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia tai ya kuvaa shingoni.
 
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Graifton Mushi tukio hilo limetokea leo saa 4 asubuhi ambapo marehemu alifunga tai juu ya kitanda chake.
 
Alisema kuwa marehemu alikuwa akisoma kozi cha Cheti cha Awali cha Utawala katika Chuo hicho.
 
Mushi aliongeza kuwa chanzo cha kifo hicho hakijulikani na Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kujua nini kilimfanya mwanachuo huyo kuchukua maamuzi hayo yaliyoacha simanzi katika jamii yake na Chuo kwa ujumla.
 
Alitoa wito kwa wanachuoni kuomba ushauri kwa viongozi wao Chuo au wa kiroho pindi wanapokuwa na matatizo binafisi kwani kujiua sio suluhisho la matatizo bali ni kuwaongezea walezi wao shida na majonzi zaidi.
Mushi alisema kuwa mwili wa marehemu umehifahiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete.
Naye Mkurugenzi wa  Chuo hicho Dkt. Ramadhani Marijani alitoa wito kwa wanachuo kuwa watulivu wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi wa sababu zilizopelekea mwanachuo huyo kuchukua maamuzi yaliyoacha simamazi sio tu kwa familia yake bali hata kwa Jumuiya nzima ya Uhazili.
Alisema kuwa ni vema kama kuna mwanachuo yoyote anakuwa na tatizo au msongo wa mawazo kuwaeleza viongozi wake wawe wa Serikali ya Wanafunzi, Mama Mlenzi, Mshauri wa Wanachuo au Mkurugenzi mwenye ili waweze kusaidia katika ushauri utakaowapa ufumbuzi kuliko kuchukua maamuzi ya haraka.

CHUO CHA MAFUNZO YA KIJESHI MONDULI YAZINDUA KOZI MPYA YA SAYANSI YA KIJESHI

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 


Katibu Mkuu Wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Florens Turuka akisalimia na Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddy Kimanta
mara  baada ya kuwasili katika chuo cha mafunzo ya kijeshi Mondoli(TMA) kwa ajili ya uzinduzi wa shahada ya kwanza ya mafunzo ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo leo(Picha na Pamela Mollel Arusha)

  Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Tanzania Jenerali Vanance Mabeyo  akisalimiana na Kaimu Mkuu wa  chuo cha uhasibu Arusha Dokt Faraji Kasidi, katikati ni Mkuu wa chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA), Dokta Paul Massao 

Katibu mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Florens Turuka akisalimia Generali Maj Othaman
mara  ya kuwasili katika chuo cha mafunzo ya kijeshi Mondoli(TMA) kwa ajili ya uzinduzi wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo


Katibu mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa Florens Turuka akisalimiana na Dr. Adolf B. Rutayuga ambaye ni kaimu mtendaji mkuu wa NACTE.

Katibu mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa Florens Turuka akizungumza katika uzinduzi wa  uzinduzi wa shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo


Mkuu wa majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo akitoa hotuba fupi katika halfa ya uzinduzi wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo


 Meja jenerali Paul Peter Masao ambaye ni mkuu wa chuo cha mafunzo ya maafisa wanafunzi jeshi la ulinzi la Tanzania(TMA).

 Mwenyekiti wa Bodi ya chuo cha uhasibu Arusha Bi.Rukia Adam akisoma maelezo mafupi  juu ya uzinduzi wa wafunzo ya shahada ya kwanza ya sayansi ya kijeshi inayotekelezwa na chuo cha uhasibu Arusha kwa kushirikiana na Chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA). 


Kaimu mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha, Dokta Faraji Kasidi akizungumza katika uzinduzi huo ambapo  alisema mahusiano kati yao na chuo hicho cha kijeshi yameanza muda mrefu ambapo wao wamekuwa wakifundisha askari hao mafunzo ya kiraia.
 

kushoto aliyevalia suti ni Profesa Johannes Monyoambaye aliwahi kuwa mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha(IAA)
 Wanafunzi  wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo leo
Maafisa wa jeshi wakitumbuiza wata wa uzinduzi wa wafunzo ya sayansi ya kijeshi.
 Picha ya pamoja


Na Pamela Mollel,Monduli

Katibu Mkuu wa wizara ya ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dokta Florens Turuka amesema kuwa jeshi hilo hivi sasa limejipanga katika kukabiliana na changamoto za ulinzi na usalama kwa kuwapatia askari wake mafunzo maalumu ya sayansi ya kijeshi. 

Aliyasema hayo Jana wakati akizungumza katika uzinduzi wa shahada ya kwanza ya sayansi ya kijeshi inayotekelezwa na chuo cha uhasibu Arusha kwa kushirikiana na Chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA). 

Alisema kuwa, kumekuwepo na matishio mengi ambayo yamekuwa yakijitokeza Kwa namna tofauti ambapo hivi sasa matishio hayo yamegeuka na kuhamia kwenye mitandao, hivyo kama jeshi wana wajibu wa kujipanga zaidi kwa kuwaandaa maaskari ili waweze kukabiliana na hali hiyo mahali popote. 

Dokta Turuka alisema kuwa, wao Kama jeshi ni wajibu wao kujipanga mapema kwa kuangalia namna ya kuwajengea uwezo hasa katika maswala ya sayansi na teknolojia ili kuboresha ulinzi na usalama hapa nchini. 

Kwa upande wa Mkuu wa majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo alisema kuwa wamekuwa wakitoa mafunzo hayo kwa maaskari wake kulingana na mabadiliko ya kidunia hasa katika maswala ya sayansi na teknolojia kwani ni eneo ambalo linahitaji elimu kubwa zaidi. 

Alisema kuwa, ni lazima wasonge mbele na kwenda na wakati kwani wasipofanya hivyo watabaki nyuma na kamwe hawataweza kukabiliana na vitisho vilivyopo  hivi sasa. 

Naye Mkuu wa chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA), Dokta Paul Massao alisema kuwa, wamekuwa wakitoa masomo ya kijeshi na kiraia ili kuwaandaa vijana katika hatua ya ngazi za  juu zaidi  kielimu  ambapo kwa kuanzia kozi hiyo watahiniwa  158  wataanza kozi hiyo mapema. 


Kwa upande wa Kaimu mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha, Dokta Faraji Kasidi alisema kuwa, mahusiano kati yao na chuo hicho cha kijeshi yameanza muda mrefu ambapo wao wamekuwa wakifundisha askari hao mafunzo ya kiraia ambayo yamekuwa yakileta manufaa makubwa Sana. 

Mwisho.