Social Icons

Friday 10 November 2017

VYUO VISUMBUFU MIKOPO YA WANAFUNZI KUFUNGIWA

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 
 Imeandikwa na Maulid Ahmed, Dodoma
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo wa Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.
SERIKALI imeviagiza vyuo vyote vya elimu ya juu kusajili wanafunzi, kuwapatia fedha zao za mikopo na watakaowasumbua watafungiwa.
Aidha imesema mpaka sasa wanafunzi 29,578 wa mwaka wa kwanza wameshapelekewa fedha zao za mikopo walikodahiliwa. Hayo yalibainishwa jana bungeni na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako wakati akitoa kauli ya serikali kuhusu udahili na utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2017/2018.
Kauli hiyo ilitokana na Bunge kuiagiza serikali kutoa kauli kuhusu udahili na utoaji wa mikopo kwa wanafunzi hao kutokana na mwongozo wa Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata (CCM).
“Serikali haitasita kuchukua hatua kali ikiwemo kuvifungia vyuo vitakavyoleta usumbufu usio wa lazima kwa wanafunzi na kuwafanya wapoteze muda ambao wanapaswa wautumie kwa masomo, UDOM (Chuo Kikuu cha Dodoma) na Chuo cha Mwalimu Nyerere wana urasimu kupokea wanafunzi, Chuo Kikuu Mwenge nimeona kinawalazimisha wanafunzi kubadilisha kozi na wanawaambia kozi zimejaa wakati waliomba na wakapata...tutavifungia vyuo vyote vinavyosumbua wanafunzi na kuwafanya wawe wazururaji mitaani,” alisema.
Profesa Ndalichako ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na Kurugenzi ya Elimu ya Juu ya Wizara ya Elimu kufuatilia kwa karibu mambo yanayoendelea vyuoni wakati wanafunzi wanaripoti na kuwabainisha wote wanaokiuka taratibu na kuwanyima wanafunzi haki yao ya kusoma programu wanazotaka.
Alisema kwa wanafunzi walioripoti vyuo tofauti na mikopo yao iliyopelekwa vyuo vingine, mikopo yao itahamishiwa kwenye vyuo walivyodahiliwa baada ya kupokea uthibitisho kutoka katika vyuo vilivyowapokea.
Alisema hadi Novemba 07 wanafunzi 29,578 wa mwaka kwanza walikuwa wamepangiwa mikopo kati ya wanafunzi 30,000 wanaostahili. Alisema serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Ellimu ya Juu imepanga kutumia Sh bilioni 427.54 kugharamia mikopo kwa wanafunzi 122,623 ambapo 30,000 ni wa mwaka wa kwanza na 92,623 ni wanaoendelea na masomo.
Katika robo ya kwanza ya mwaka huu, Wizara ya Elimu imepokea Sh bilioni 147.06 kwa ajili ya ada za wanafunzi hao kugharamia chakula, malazi, vitabu, viandikia na mahitaji ya masomo.
CHANZO HABARI LEO

No comments: