Social Icons

Tuesday 31 January 2017

CHUO CHA AFRICA GRADUATE UNIVERSITY CHAWATUNUKU PhD WANAOFANYA KAZI ZA JAMII NCHINI

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.

Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate University  cha jijini Dar es Salaam, Profesa Stiven Nzowa, akiongoza mahafali ya kuwatunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD) wanaharakati na watumishi wa mungu nane pamoja na wengine kadhaa waliotunukiwa Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili HDD Dar es Salaam jana.
 Mwanaharakati wa Haki za Watoto ambaye ni Rais wa Tanzania Music Foundation Dk.Donald Kisanga aliyetunukiwa PhD ya masuala ya Usimamizi na Uongozi wa Biashara akiwa kwenye mahafali ya 30 ya Chuo cha Africa Graduate University yaliyofanyika Dar es Salaam jana.
 Askofu Dk. Godfrey Mallasy wa Kanisa la Tanzania Fellowship of Churches, akielezea kazi mbalimbali alizofanya kabla ya kutunukiwa tuzo hiyo.
 Waliotunukiwa tuzo wakiwa na furaha katika picha ya pamoja.
 Wageni waalikwa wakiwa na Mama Askofu Dk.Godfrey Mallasy, Debora Mallasy (mwenye kofia), alikuwepo kushuhudia mume wake akitunukiwa tuzo hiyo.
 Meneja Programu na mshereheshaji katika mahafali hayo, 
Lucy Wilson akiwa kazini.
 Watunukiwa tuzo hao wakiingia ukumbuni.
 
 Wimbo wa Taifa ukiimbwa.Katikati ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Salum Hamdun ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali hayo. Kushoto ni Mkuu wa chuo hicho, Profesa Stiven Nzowa na kulia ni mke wa Makamu Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate University, Profesa Timothy Kazembe.

 Mama Askofu Dk.Godfrey Mallasy, Debora Mallasy akiomba kabla ya kuanza kwa mahafali hayo.
 Mkaguzi wa Polisi (ASP) Ezekiel Kyogo akionesha moja ya kitabu alichokiandika chenye manufaa kwa jamii. Kyogo alitunukiwa PhD.
 Meneja Takwimu Mkoa wa Arusha Margaret Mutaleba, akieleza kazi alizozifanya katika jamii.
 Wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla hiyo.
 Wasanii wa Bendi ya Jordan wakitumbuiza katika mahafali hayo.
 Mwanahabari Tumaini Msowoya, akieleza kazi alizoziandika ambapo zimekifanya chuo hicho kumtunuku Tuzo hiyo ya Heshima.
 Watoa huduma katika mahafali hayo, wakiwa katika picha ya [pamoja na Meneja Programu, Lucy Wilson.

Makamu Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate University, Profesa Timothy Kazembe (kulia), akimtunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD), Askofu Dk. Godfrey Mallasy katika mahafali hayo.
 Makamu Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate University, Profesa Timothy Kazembe (kulia), akimtunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD), Meneja Takwimu Mkoa wa Arusha, Margaret Mutaleba.
  Makamu Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate University, Profesa Timothy Kazembe (kulia), akimtunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD), Godwin Maimu.
 Makamu Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate University, Profesa Timothy Kazembe (kulia), akimtunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD), Donald Kisanga.
  Makamu Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate University, Profesa Timothy Kazembe (kulia), akimtunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD), Mwanahabari Tumaini Msowoya.
 Furaha na tabasamu baada ya kutunukiwa tuzo hiyo.
 Watunukiwa tuzo hizo, Dk.Donald Kisanga (kushoto) na Mkaguzi wa Polisi (ASP), Ezekiel Kyogo (kulia), wakiwa na jamaa zao baada ya kutunukiwa tuzo hiyo.
Viongozi wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Dk.Godwin Maimu (kushoto) na Dk.Donald Kisanga wakiwa katika picha ya pamoja.

Na Dotto Mwaibale

CHUO cha Africa Graduate University  cha jijini Dar es Salaam kimewatunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD) wanaharakati na watumishi wa mungu nane pamoja na wengine kadhaa waliotunukiwa Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili HDD.

Watumishi waliotunukiwa tuzo hizo za heshima ni wale waliotoa mchango mkubwa kwa kufanya shughuli mbalimbali za kujitolea za kijamii na zikaleta manufaa kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika mahafali ya 30 ya chuo hicho chenye makao makuu yake Sierra Leone, Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Stiven Nzowa alisema kila mwaka chuo hicho kimekuwa kikitoa Tuzo za heshima na Shahada za Uzamili kwa watanzania waliotoa mchango wa kusaidia jamii katika shughuli mbalimbali.

"Tunao watunuku tuzo hizi tuzo za heshima ni watu waliokuwa na umri wa miaka 60 ambao wanafanya kazi za kijamii katika nyumba za ibada kwa zaidi ya miaka 15 na kuendelea na wale ambao umri wao ni miaka 40 hadi zaidi na wenye shahada" alisema Profesa Nzowa.

Wakizungumzia kazi walizozifanya katika jamii Askofu Dk. Godfrey Mallasy wa Kanisa la Tanzania Fellowship of Churches alisema amefanyakazi nyingi za kijamii ikiwemo kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima na kubwa zaidi kwa kipindi cha miaka 20 amekuwa akifanya mkesha mkubwa wa kuliombea taifa amani na yeye akiwa ni mhasisi.

"Kazi hii ya kuliombea taifa amani tulianza mwaka 1997 na tumeweza kupeleka huduma hiyo hadi Zanzibar ambako kumefanyika maombi hayo kwa miaka saba na kuifanya Tanzania kuwa na amani" alisema Dk. Mallasy.

Mwanaharakati wa Haki za Watoto ambaye ni Rais wa Tanzania Music Foundation Dk.Donald Kisanga aliyetunukiwa PhD ya masuala ya Usimamizi na Uongozi wa Biashara alisema amefanya kazi nyingi za kijamii ikiwa pamoja na kuishawishi serikali kukagua fedha zinazotolewa na wahisani kwenye taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na kuwatunza watoto yatima baada ya kubaini baadhi yake zimekuwa zikifuja fedha bila ya kuwasaidia walengwa.

Mwingine aliyetunukiwa tuzo hiyo ya heshima ni Meneja Takwimu Mkoa wa Arusha Margaret Mutaleba ambaye pamoja na kufanya shughuli nyingi za kijamii pia ndiye aliyemshauri Rais Dk. John Magufuli kuhusu mpango wa kufanya usafi ambao unaendelea kutekelezwa nchini kote.

Mbali na watu hao kutunukiwa tuzo hiyo ya heshima yupo mwanahabari mahiri wa gazeti la Mwananchi, Tumaini Msowoya ambaye ametunukiwa PhD kutokana na kufanya kazi mbalimbali za kijamii kupitia kalamu yake ambazo zimeleta mrejesho mkubwa kwa walengwa na kuweza kusaidiwa.

Waliotunukiwa tuzo ya heshima ya udaktari ni Donald Kisanga, Mlute Nyasa, John Pallangyo, Wilson Nyiti na Godwin Maimu.

Wengine ni Askofu Dk. Godfrey Mallasy, Ofisa wa Jeshi la Polisi Ezekiel Kyogo, Mtakwimu Margaret Mutaleba na Mwanahabari Tumaini Msowoya.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

No comments: