Social Icons

Thursday 10 March 2016

DK.KIGWANGALLA AKUTANA NA MADAKTARI WALIOHITIMU MAFUNZO KWA VITENDO 2014/15

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla amekutana na baadhi ya Madaktari waliohitimu mafunzo kwa vitendo kipindi cha 2014/2015 waliofika katika Wizara hiyo kwa lengo la kujua hatima na mustakabali wa mambo mbalimbali ikiwemo suala la ajira.
Madaktari hao walioweza kuonana na Dk. Kigwangalla ni baadhi tu ya wawakilishi wa Madaktari wengine ambapo kupitia viongozi wao wamebainisha kuwa, kuwa kama wazarendo wapo tayari kuisaidia Serikali katika suala la tiba nchini hasa kwendana na hali ya kauli mbiu ya hapa kazi hivyo kupitia mazungumzo yao hayo na Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla na jopo la viongozi wa Wizara hiyo, madai yao na masuala mengine wana Imani kubwa madai yao yatashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi.
kigwangalla ioNaibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla (katikati) akifuatilia mkutano huo uliowakutanisha Madaktari waliohitimu mafunzo kwa vitendo 2014/2015 (waliokaa upande wa kushoto). Wengine waliokaa upande wa kulia ni viongozi watendaji wa ngazi za juu wa Wizara hiyo wakifuatilia mkutano huo. Madaktari hao walifanya mkutano huo kwa lengo la kutaka kufahamu masuala mbalimbali ikiwemo suala la ajira.
Kigwangalla34Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla (wa pili kutoka kushoto) akitoa ufafanuzi kwa wanafunzi hao juu ya mipango ya Wizara hiyo na namna ilivyojipanga ikiwemo kushughulikia suala lao hilo ambalo ni la kiutawala zaidi.
kigwangalla99Viongozi wa Wizara ya Afya wakiwemo Makatibu wakuu na wakuu wa vitengo wakifuatilia mkutano huo kwa makini
kigwangalla qBaadhi ya Madaktari waliohitimu mafunzo kwa vitendo wa mwaka wa 2014/2015 wakitoa maoni yao pamoja na mambo mbalimbali waliyoyawakilisha kwa Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla pamoja na viongozi wa kutoka Wizara hiyo (Hawapo pichani).
kigwangalla cvBaadhi ya Madaktari hao waliohitimu mafunzo kwa vitendo mwaka 2014/15
kigwangalla 87Mkutano huo ukiendelea..
kigwaNaibu Waziri Afya, Dk. kigwangalla akipeana mkono na baadhi ya viongozi wa Madaktari hao waliohitimu mafunzo kwa vitendo 2014/15, mara baada ya mkutano wao huo.
kiganngwalla4Hapa Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla aliombwa kupata picha ya 'selfie' ya ukumbusho na Madaktari hao waliohitimu mafunzo kwa vitendo 2014/15
kigwangalla3"Selfie na Naibu Waziri": Baadhi ya Madaktari waliohitimu mafunzo kwa vitendo 2014/15 walipata wasaha wa kupiga picha ya kumbukumbu na Naibu Waziri. Naibu Waziri ambaye naye ni Daktari, Madakatri hao walifurahia nafasia hiyo kwani ni kumbukumbu muhimu sana kwao kama walivyodai wakati wa picha hiyo.
kigwangalla 2Baadhi ya viongozi wa Madaktari waliohitimu mafunzo kwa vitendo mwaka 2014/15 wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Afya Dk. Kkigwangalla.
Kigwangalla9Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Wizara hiyo pamoja na uongozi wa Baadhi ya Madaktari waliohitimu Mafunzo kwa vitendo wa mwaka 2014/15 pamoja wahitimu hao katika picha ya pamoja nje ya Wizara hiyo. (Picha zote na Andrew Chale,Modewjiblog).

No comments: