Social Icons

Saturday 7 March 2015

KINANA AKUTANA NA WANAFUNZI WA VYUO VYA ELIMU YA JUU DODOMA‏


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa nje ya ukumbi wa NEC maarufu kama white house mjini Dodoma tayari kwa kukutana na wanafunzi wa Shirikisho la vyuo vya elimu ya juu mkoani Dodoma.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu mkoani Dodoma kabla ya kuingia kwenye mkutano kwenye ukumbi wa mikutano wa NEC maarufu kama White House,CCM makao makuu Dodoma.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimia na Viongozi mbali mbali wa CCM mkoa wa Dodoma.
 Katibu Mtendaji wa Shirikisho a Vyuo vya Elimu ya Juu nchini Ndugu Christopher Ngubiagai akizungumza wakati mkutano wa shirikisho la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu Dodoma.
 Wanafunzi kutoka vyuo vya elimu ya juu wakisikiliza kwa makini hoja mbali mbali zilizokuwa zikijadiliwa wakati wa mkutano huo.
 Judith Haule kutoka Chuo cha Mipango Dodoma akizungumzia masaula ya ajira na changamoto zake na mfumo wa elimu unaosababisha watu waamini katika kuajiriwa zaidi na si kujiajiri.
 Thomas Mathias kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma akizungumza kwenye mkutano wa shirikisho la vyuo vya elimu ya juu Dodoma na kuzungumzia masauala mbali mbali yanayohusu mikopo na kuwawezesha wanafunzi wengi kupata fursa ya kusoma elimu ya juu nchini.

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.

No comments: