Social Icons

Tuesday 8 April 2014

Wanafunzi 2,006 hawajaripoti kidato cha kwanza mkoani Singida


Shukuru Kawambwa
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa.
Na Nathaniel Limu, Singida
JUMLA ya wanafunzi 2,006 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu mkoani hapa bado hawajaripoti katika shule walizopangiwa.
Hayo yamesemwa hivi karibuni na Afisa Kazi Sekretariati mkoani Singida,Jacob Elias wakati akitoa taarifa ya usajili wa wanafunzi kidato cha kwanza mwaka huu mbele ya kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Chuo cha Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) mjini Singida.
Amesema wanafunzi hao ambao bado hawajaripoti hadi sasa ni sawa na asilimia 19 ya wanafunzi wote 10,802 waliofaulu mtihani wa taifa wa kumaliza shule za msingi.
Akifafanua,Jacob amesema wilaya ya Manyoni inaongoza kwa wanafunzi 585 ambao hawajaripoti kuanza kidato cha kwanza hadi sasa.
“Manyoni inafuatiwa na Wilaya ya Ikungi ambayo wanafunzi 503 hawajaripoti kuanza kidato cha kwanza hadi sasa.Iramba 318, Manispaa ya Singida 270, Singida vijijini 238 na Mkalama 92″, amesema Jacob.
ZAIDI SOMA HAPA>>>

No comments: