Social Icons

Monday 14 April 2014

Serikali kuwazawadia wanafunzi na shule za msingi na sekondari zinazofanya vizuri


ShukuruKawambwa
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dkt. Shukuru Kawambwa.
Na Mwandishi Wetu
Katika kutekeleza Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) katika sekta ya Elimu, Serikali itawazawadia wanafunzi na shule zilizofanya vyema katika mitihani ya Elimu ya msingi na Sekondari.
Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam Jumatatu April 14, 2014 na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dkt. Shukuru Kawambwa alipozungumzia na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Wiki ya Elimu.
Kwa mujibu wa Dkt. Kawambwa, maadhimisho ya wiki hiyo ya Elimu itakayoanza Mei 3 hadi 9 mwaka huu ni ya kwanza nchini na yanalenga katika kutambua juhudi za kuendeleza ubora wa Elimu nchini.
“Pamoja na malengo mengine, wiki hii italenga katika kutoa motisha na zawadi kwa shule na wanafunzi waliofanya vizuri ikiwa ni utekelezaji wa wa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa,” alisema Waziri Kawambwa.
Miongoni mwa malengo ya BRN katika kukuza ubora wa elimu nchini ni pamoja na kutoa motisha kwa walimu na wanafunzi wa shule zinazoonekana kuvuka viwango vya kukuza ubora.
Kwa mujibu wa Dkt. Kawambwa, maadhimisho hayo yatakayofanyika mjini Dodoma yatazinduliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda pia yatafungwa na Rais Jakaya Kikwete.
Kwa mujibu wa Waziri Kawambwa, maadhimisho hayo yataanzia katika ngazi ya Wilaya, Mikoa na kasha kufanyika Kitaifa.
Alisema viongozi wote wa Mikoa na Wilaya wamekwishapewa taarifa ya kufanya maandalizi hayo ili kufanikisha sherehe hizo.
BRN ni Mpango wa utekelezaji wa miradi mikubwa chini ya Ofisi ya Rais ukilenga kuhakikisha kuwa miradi iliyopewa kipaumbele inapewa fedha za kutosha ili kupata maendeleo ya haraka

No comments: