Social Icons

Monday 3 February 2014

NAIBU WA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI Mhe. JENISTA MHAGAMA ATEMBELEA BODI YA MIKOPO


 Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Jenista Mhagama (MB) akikaribishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Bw. George R.W. Nyatega (kushoto)) katika Ofisi za Bodi hiyo zilizoko Mwenge,  Dar Es Salaam.
 Mh.Naibu Waziri akipeana mkono na baadhi ya wawakilishi wa Menejimenti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.


Naibu Waziri Mhe. Jenista Mhagama (kushoto) wakiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Bw. Nyatega, wakifuatilia mada ya Utoaji Mikopo iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Uchambuzi na Utoaji Mikopo Bw. Onesmus Leizer (hayupo pichani)

Naibu Waziri alipata pia bahati ya kukutana na mmoja wa wanafunzi wake Bi. .Sarah Fihavango ambaye kwa sasa ni Afisa Mikopo Mwandamizi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.
----------
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Jenista Mhagama (Mb) ametembelea ofisi za makao makuu ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu yaliyopo barabara ya Sam Nujoma Mwenge Dar Es Salaam.
Ziara hiyo inafuatia uteuzi wake uliofanywa hivi karibuni na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.
Mhe.Jenista Mhagama(Mb), ameipongeza Menejiment ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa utendaji wao wenye ufanisi ulioperekea migomo kupungua katika vyuo mbali mbali nchini, aidha Naibu Waziri amepongeza pia jitihada za Bodi ya Mikopo inayofanyika katika urejeshwaji ambayo imeperekea kupatikana kwa Bilioni 19, ambazo pia zimetumika katika ukopeshaji wa Wanafunzi wahitaji katika mwaka wa masomo 2013/14.
Katika ziara hiyo Mhe. Naibu Waziri aliambatana na Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Prof. Sylivia Temu.
Akimtambulisha Naibu Waziri kwa Menejimenti ya Bodi ya Mikopo, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Bw. George Nyatega alisema ``……ni bahati kutembelewa na Naibu Waziri ambaye bado ni mpya kwenye Wizara, kwani ni majuzi tu ndiyo  Mhe. Mhagama ameteuliwa katika Wizara hii’’.
Aidha, Bwana Nyatega alitumia fursa hiyo kumwelezea Naibu Waziri  shughuli za kila siku za  Bodi ya Mikopo ikiwa ni pamoja na historia fupi ya kuanzishwa kwa Bodi ya Mikopo, mafanikio, na changamoto zinazoikabili Bodi hiyo.

Michuzi Media group


No comments: