NA: HIDAN .O. RICCO.
Mahafali
ya saba ya Taasisi ya Teknolojia ya Dar Es Salaam imefanyika wiki
iliyopita jijini DSM ikihudhurisha wahitimu zaidi ya 500 katika ngazi
ya Astashahada, Stashahada na Shahada ya juu.
Taasisi
ya Teknologia ya Dar Es Salaam, DIT ambayo zamani ilikuwa ikijulikana
kama Chuo cha Ufundi cha Dar Es Salaam, maarufu kama Dar Tech, inayo
Idara 8 kama ifuatavyo, Idara ya Uhandisi Kompyuta, Idara ya Uhandisi
Ujenzi, Idara ya Uhandisi Migodi, Idara ya Uhandisi Umeme, Idara ya
Uhandisi Elektroniki na Mawasiliano ya Anga, Idara ya Uhandishi Mitambo,
Idara ya Sayansi na Teknologia ya Maabara, Idara ya Teknologia ya
Habari.
Wahitimu kutoka Idara mbalimbali walitunukiwa Vyeti, Diploma, na Shahada ya juu kulingana na masomo waliyochukua.
Mgeni
Rasmi katika Hafla hiyo alikuwa Mheshimiwa Waziri wa Mawasiliano,
Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbaraw, Mbunge akimuwakilisha
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mohamed
Gharib Bilal, ambaye alikuwa na udhuru.
Maandamano
ya mahafali yalianza saa 7.30 mchana kwa Wahitimu kuingia viwanja vya
michezo katika Taasisi hiyo, na Mgeni Rasmi aliwasili muda wa saa 8.00
akiongozana na jopo na Wahadhiri pamoja na Mkuu wa Taasisi Profesa John
Kondoro.
Baada
ya Mlau [Chief of Protocol] kutoa salamu za makaribisho, na kusimika
Rungu rasmi katika meza iliyoandaliwa kama inavyofanya katika ukumbi wa
Bunge, Wimbo wa Taifa uliimbwa na baadae Mkuu wa Taasisi alisoma hotuba
yake, ikifuatiwa na hotuba ya Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya
Teknolojia ya Dar Es Salaam ambaye ndie aliyemkaribisha Mgeni Rasmi
kusoma hotuba yake na baadaye zoezi la kutunuku Vyeti kuanza.
Wahitimu
wa ngazi ya cheti [Astashahada] katika fani ya Ufundi wa Teknolojia ya
Habari yaani Basic Technician Certificate in Information Technology,
ndio waliokuwa wa kwanza kutunukiwa wakifuatiwa na Idara zingine, na
hatimaye kumalizia na Wahitimu wa Shahada ya Juu.
Wahitimu
49 wa fani ya Uhandisi Ujenzi, yaani Bachelor of Engineering in Civil
Engineering ndio waliokuwa wa kwanza kutunukiwa Shahada ya juu
wakifuatiwa na 24 wa fani ya Uhandisi Kompyuta yaani Bachelor of
Engineering in Computer Engineering.
Wahitimu
wote wa Shahada ya Juu mara baada ya kutunukiwa Shahada zao walivaa
rasmi kofia zao kuashiria kwamba sasa ni wahitimu kamili, huku brass
band ya Jeshi la Magereza wakipiga wimbo maalum wa fan fair wakati
wahitimu kutoka Idara mbalimbali wakitajwa majina yao na kuinuka katika
viti vyao na kujipanga mbele ya Jukwaa la Mgeni Rasmi kupokea tuzo hizo.
Zoezi
la mwisho lilikuwa ni kutangazwa rasmi kwa Wahitimu bora wa kila Program
na Idara wanazotoka. Upande wa Stashahada walikuwa wahitimu 8 wote wa
jinsia ya kiume, na upande wa Shahada waliotunukiwa walikuwa wahitimu 5
wanne wakiwa ni wanaume na mmoja ni msichana aliyetambulika kwa jina la
Cecylia Kuguru, ambaye alishangiliwa na ukumbi mzima uliokuwa umefurika
na wazazi, walezi, wanafunzi pamoja na wageni waalikwa.
Mgeni
Rasmi Profesa Makame Mbarawa kwa Mamlaka aliyopewa alitangaza hapo hapo
kumpa scholarship ya kusoma Masters Degree mhitimu huyo katika Chuo
chochote atakachopenda.
Tamko
hilo liliongeza vifijo na nderembo uwanjani hapo huku Mgeni Rasmi
akiwahimiza wanafunzi wengine kusoma kwa bidii, kuwa wanafunzi bora na
hatimaye kujipatia nafasi kama hizo za kusomeshwa bure na Serikali.
Mhitimu
Cecylia Kuguru anatokea Idara ya Uhandishi Elektroniki na Mawasiliano
Anga, mafunzo ambayo yanamuwezesha kupata ajira na nafasi ya Juu katika
Idara ya Mawasiliano ya angani kama Control Tower ya Mawasiliano ya
ndege, meli na kadhalika.
Mwanafunzi
Mhitimu bora ndugu Elias Eliud kwa niaba ya wahitimu wenzake alitoa
neno la shukrani, na baadaye sherehe zilifungwa kwa kupigwa picha za
pamoja Wahitimu bora na Mgeni Rasmi, Wakuu wa Idara pamoja na Wageni
Waalikwa.
No comments:
Post a Comment