Social Icons

Wednesday 27 November 2013

CHUO KIKUU CHA IRINGA CHAILETEA HESHIMA TANZANIA KATIKA SHINDANO LA TUZO YA HESHIMA YA SHERIA ZA VITA




makamu Mkuu  wa  chuo   kikuu  cha Tumaini Iringa, Prof Nicholaus Bangu kushoto akipokea tuzo  ya heshima ya sheria  za vita  kutoka kwa mkuu msaidizi  wa kitivo cha sheria  Jane Massey  huku wanafunzi walioshinda  wakishuhudia  zoezi hilo  leo
Washindi  wa tuzo hiyo chuo kikuu cha Iringa wakiwa na tuzo yao kushoto ni mkuu wa chuo Prof Nicholaus Bangu  na kulia wa kwanza na mkuu msaidizi wa kitivo cha sheria Bi Jane Massey
mkuu msaidizi wa  kitivo cha  sheria chuo kikuu cha Iringa Jane  Massey akikabidhiwa tuzo ya  heshima ambayo chuo  hicho kimeshinda katika mashindano yaliyoshirikisha  nchi saba Afrika na chuo  hicho  kunyakua tuzo hiyo kwa kuwa chuo cha kwanza

Mkuu  wa chuo  cha Tumaini (  chuo  kikuu cha Iringa ) Prof Nicholaus Bangu  akionyesha tuzo ya heshima ya  sheria  za kivita ambayo chuo chake  kimeiwezesha Tanzania  kufanya  vema
Washindi  wa  tuzo hiyo  wakiwa na vyeti vyao katika picha ya pamoja na mwalimu  Dr Chachage 

Tanzania yazibagwa nchi sita barani Afrika katika mashindano ya vyuo  vikuu ya  kuwania tuzo ya heshima   ya sheria  za  vita  yaliyomalizika  hivi karibuni .

Katika  shindano hilo lililofanyika   kati ya Novemba   16-23 mwaka  huu  jijini  Arusha chuo  kikuu  cha Iringa  kiliwakilishwa na  washiriki  watatu  ambao ni Anneny Nahum ,Janeth Nagai   na Joanna Mcintype vijana  hao  waliweza kufanya  vema  kiasi  cha  kuiwezesha nchi ya Tanzania kuibuka mshindi  wa kwanza wa  tuzo hiyo.

Wakizungumza leo chuoni  hapo katika hafla  fupi ya kukabidhi  tuzo hiyo kwa uongozi wa  chuo hicho ,washirikia hao  walisema  kuwa  ushindi  huo  umetokana na ushirikiano  ulioonyeshwa na nidham iliyotukuka miongoni mwao.

Hata  hivyo  walisema  kuwa  tuzo  hiyo  ni  heshima kubwa kwa Tanzania  na ni heshima kwa  chuo  hicho .

mkuu msaidizi wa  kitivo cha  sheria chuo kikuu cha Iringa Jane  Massey alisema  kuwa washiriki hao  wamepata kushinda kutokana na kuonyesha  uwezo wa hali ya  juu katika mashindano hayo na  kuwa  heshima kubwa ambayo  chuo hicho  imepata  ni jambo na kujivunia na kumshukuru Mungu  pia.

ZAIDI SOMA HAPA



No comments: