Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar, ni taasisi ya Serikali  iliyoanzishwa kwa sheria namba 8 ya mwaka 2011. 
Mamlaka
 ya Viwanja vya Ndege inatangaza nafasi za Kazi katika maeneo 
yaliyoainishwa hapo chini, kwa wazanzibar wenye sifa zinazohitajika.
1. OFISA USALAMA DARAJA LA I I (AVIATION SECURITY OFFICER GRADE II)  Nafasi 10  Unguja
Sifa ya kuingia kazini
Mwenye
 Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika 
fani ya Mifumo ya Kompyuta (IT) au Sheria au Sayansi ya Jamii au Utawala
 au Menejimemti ya Rasilimaliwatu  kutoka chuo kinachotambuliwa na 
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 
1. OFISA USALAMA MSAIDIZI DARAJA LA III (AVIATION SECURITY ASSISTANT OFFICER GRADE III) Nafasi 40 Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye
 Stashahada ya Mifumo ya Kompyuta (IT) au Sheria au Sayansi ya Jamii au 
Utawala au Menejimemti ya Rasilimaliwatu  kutoka chuo kinachotambuliwa 
na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 
2. MHANDISI MITAMBO (MECHANICAL ENGINEER) Nafasi 1  Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Kuajiriwa
 mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili 
katika fani ya Mitambo au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika 
chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).
3.MHANDISI MAJENGO (CIVIL ENGINEER) Nafasi 1  Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Kuajiriwa
 mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili 
katika fani ya Ujenzi au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika 
chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).
2. MHANDISI UMEME (ELECTRICAL ENGINEER) Nafasi 1  Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
Kuajiriwa
 mwenye Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili 
katika fani ya Umeme au fani nyengine inayolingana nayo kutoka katika 
chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).
3. OFISA MAZINGIRA (ENVIRONMENTAL OFFICER) Nafasi 1  Unguja 
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye
 Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika 
fani ya Sayansi/Sanaa ya Mazingira au fani nyengine inayolingana nayo 
kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
 (SMZ).
4. FUNDI MCHUNDO UMEME DARAJA LA  III ( Nafasi 1Unguja na 1 Pemba )
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye
 Stashahada ya kawaida au FTC katika fani ya umeme au cheti chengine 
kinachofanana na hicho kutoka katika taasisi inayotambulika na serikali.
5. FUNDI SANIFU UMEME DARAJA LA  III ( Nafasi 3 Unguja )
Sifa za Kuingilia Kazini
 Mwenye
 cheti katika fani ya Umeme au fani nyengine inayolingana nayo kutoka 
katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar 
(SMZ). 
6. FUNDI SANIFU KUCHONGA (CARPENTER) Nafasi 1 Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
 Mwenye
 cheti katika fani ya ufundi  kuchonga au fani nyengine inayolingana 
nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya 
Zanzibar (SMZ). 
7. FUNDI SANIFU KUCHONGA (ALLUMINIUM) Nafasi 1 Unguja
Sifa za Kuingilia Kazini
 Mwenye
 cheti katika fani ya ufundi  kuchonga au fani nyengine inayolingana 
nayo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya 
Zanzibar (SMZ). 
8. FUNDI MCHUNDO BOMBA (PLUMBER) DARAJA LA  III ( NAFASI 1 UNGUJA)
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye
 Stashahada ya kawaida au FTC katika fani ya Ufundi Bomba au cheti 
chengine kinachofanana na hicho kutoka katika taasisi inayotambulika na 
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). 
9. MUEGESHA NDEGE MSAIDIZI DARAJA LA III (nafasi  6 Unguja, 2 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye
 cheti cha kidatu cha nne pamoja na cheti cha masomo ya Uegeshaji wa 
Ndege (Appron Management)  au  cheti  kinachofanana na hicho ambacho 
kimetolewa na Mamlaka inayotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya 
Zanzibar (SMZ). 
10. KATIBU MUKHTASI DARAJA LA III ( Nafasi 3 Unguja)
Sifa za kuingilia kazini 
Mwenye Diploma/Stashahada ya fani ya Uhazili kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
11. OFISA BIASHARA DARAJA LA II ( nafasi 1 Unguja na 1 Pemba)
Sifa za Kuingilia Kazini
Mwenye
 Shahada ya Kwanza/Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika 
fani ya Masoko, Biashara, Utawala na Uchumi, Sheria za Kibiashara au 
fani nyengine inayolingana nazo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na 
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
12. MHASIBU MSAIDIZI DARAJA LA III (nafasi 1 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye Stashahada ya kawaida ya Uhasibu au Uongozi wa Fedha kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
13. MHUDUMU VIP DARAJA LA II (nafasi 2 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini 
Mwenye
 cheti cha kidatu cha nne au sita na hicho kutoka katika mamlaka 
inayotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Mwenye uzoefu
 wa kuwahudumikia viongozi atapewa kipau mbele.
14. DEREVA DARAJA LA III (nafasi 1 Pemba)
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye
 cheti cha Kidato cha nne aliyefaulu na kupata leseni ya gari kutoka 
katika Mamlaka inayotoa leseni na kutambuliwa na Serikali ya Mapinduzi 
ya Zanzibar. 
15. a) OFISA WA MIFUMO YA KOMPYUTA DARAJA LA II (System Administrator)  nafasi moja Unguja na moja Pemba
b) OFISA WA MITANDAO YA KOMPYUTA  DARAJA LA II (Net Works Engineer) nafasi moja Unguja.
c) OFISA WA KUKIMU MIFUMO YA KOMPUTA (IT Service/Support Engineer) nafasi moja Unguja
d) OFISA  MUENDELEZAJI MIFUMO YA KOMPUTA (System Developer) nafasi mbili Unguja
Sifa za kuingilia kazini
Mwenye
 Shahada ya Kwanza /Stashahada ya Juu au Stashahada ya Uzamili katika 
fani ya Sayansi ya Kompyuta/habari ya Kompyuta au fani nyengine 
inayolingana nazo kutoka katika chuo kinachotambuliwa na Serikali ya 
Mapinduzi ya Zanzibar.  
• Kufanya kazi nyengine zinazolingana na kazi yake kama atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.
Jinsi ya Kuomba 
Barua za maombi  zielekezwe kwa:-
Mkurugenzi Mkuu 
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
S.L.P 4742
Zanzibar 
Barua
 hizo ziambatanishwe na taarifa binafsi ya muombaji (CV), Vivuli vya 
Cheti cha kuzaliwa, Kitambulisho cha Ukaazi cha Zanzibar na vyeti  vya 
masomo.
Siku ya mwisho ya kupokea maombi hayo ni siku ya Jumatano ya tarehe 04/08/2017.

No comments:
Post a Comment