Social Icons

Tuesday 15 November 2016

WAANZISHAJI VYUO HOLELA VYA AFYA WAFUNGIWE

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 


Na CATHERINE SUNGURA
KIBAHA
Baraza  la Wauguzi na Wajunga nchini wametakiwa kutowaonea aibu wale wote wanaoanzisha vyuo vya afya kama mradi wa kujiingizia fedha bila ya kuwa na taaluma hiyo kwani kunapelekea kuhatarisha Maisha na afya za watanzania.
Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati akiweka jiwe la msingi katika jengo la kituo cha kuendeleza wauguzi na wakunga kitaaluma nchini lililopo mjini kibaha Pwani.
“Hatusemi wasianzishe vyuo,bali vyuo vyote viwe vyenye hadhi ya kutoa wataalam stahili ,visajiliwe na vikaguliwe mara kwa mara ili vizalishe wauguzi wenye sifa na ujuzi stahili,uuguzi siyo ujasiliamali,hakikisheni mnavifungia vyuo vyote feki ili tuweze kudhibiti utitiri huu” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy alisema hivi sasa kumekuwepo na utitiri wa vyuo vingi vya uuguzi ambavyo havijasajiliwa na havizalishi wauguzi ambao wanastahili kuajiriwa kwenye sekta ya afya na hivyo kuhakikisha wanasimamia taaluma hiyo na kuvifungia mara moja vyuo vilivyokosa sifa.
Waziri Ummy alisema kuwa serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa unaofanywa na wauguzi katika hospitali zote nchini hivyo maboresho yatafanyika na kuhakikisha  upatikanaji wa vitendea kazi kwa wauguzi.
“Asilimia 80 za kazi zote katika hospitali zetu nchini zinafanywa na wauguzi na wakunga hivyo Serikali imesikia kilio chenu na tutahakikisha tatizo hili tunalitatua” alisema Ummy.
Hata hivyo Waziri Ummy  aliwataka wauguzi kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia maadili na  viapo vyao vya kitaaluma kwa maendeleo ya  Afya nchini.
Kwa upande wa  Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga nchini Bi. Lena Mfalila alisema jengo hilo linajengwa  kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza limegharimu pesa ya kitanzania shilingi bilioni 2.2.
Aidha Bi. Mfalila alisema kuwa ujenzi wa kituo hicho ulianza Desemba 2015 kwa awamu ya kwanza na kiinatarajiwa kukamililika na kuanza matumizi yake Januari2017 .
MWISHO.


No comments: