Social Icons

Friday 3 June 2016

TAARIFA RASMI KWA UMMA: KUAHIRISHWA KWA USAILI WA NAFASI ZA KAZI KWA TANGAZO LILILOTOLEWA TAREHE 1 JUNI, 2016

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 


KUAHIRISHWA KWA USAILI WA NAFASI ZA KAZI KWA TANGAZO LILILOTOLEWA TAREHE 1 JUNI, 2016

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Tanzania Metrological Agency (TMA), Tanzania Meat Board (TMB), The Local Government Training Institute (LGTI) na Registration, Insolvency And Trusteeship Agency (RITA) alitoa tangazo katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira la kuita kwenye usaili tarehe 1 Juni, 2016 waombaji wa kazi waliowasilisha maombi na kukidhi vigezo kwa taasisi zilizoanishwa hapo juu.

Kupitia tangazo hili Waombaji kazi wote waliotangaziwa kuitwa kwenye usaili kwa tangazo hilo wanafahamishwa kuwa usaili huo umeahirishwa mpaka watakapotangaziwa tena hapo baadaye.  

Kwa Matangazo ya nafasi za kazi yaliyotolewa mnamo tarehe 6 Mei, 2016, 11 Mei, 2016, 18 Mei, 2016 na tarehe 26 Mei, 2016 nayo waombaji kazi watakaokidhi vigezo watataarifiwa hapo baadae kuhusu mchakato wake unavyoendelea.

Aidha, Kupitia tangazo hili, Sekretarieti ya Ajira kwa niaba ya Serikali inaomba radhi waombaji kazi wote waliowasilisha maombi na wale waliokuwa wamejiandaa kuhudhuria usaili huo kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na


X.M. DAUDI
KATIBU
Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma.


No comments: