Social Icons

Monday 10 August 2015

Wanafunzi waliosoma St Joseph Cathedral High School wakutana jijini Dar es salaam, kuzindua chama Septemba 26/2015 karimjee‏

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

1

Richard Rugimbana Mwenyekiti wa Chama cha Wanafunzi waliosoma katika shule ya (St Joseph Cathedral High School Alumn )kuanzia mwaka 1940 - 2014 akizungumza katika mkutano wao uliofanyika shuleni hapo jana wakati wa kikao chao kikilchojadili mipango mbalimbali ikiwamo kuanzisha mfuko wa Elimu utakaosaidia kuwasomesha wanafunzi wa shule hiyo wenye mahitaji maalum ikiwemo kuwapatia Scholaship katika vyuo mbalimbali.

Chama hicho kinatarajiwa kuzinduliwa rasmi Septemba 26 kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam , Katika kufanikisha uzinduzi huo kadi maalum zimeandaliwa ambazo zitauzwa shilingi 50.000 kwa mtu mmoja , 100.000 kwa watu wawili na meza za watu kumi kila moja zitakazouzwa kwa kiasi cha shilingi 1.000.000. Katika Picha kushoto ni Katibu wa Chama hicho Bwa.Collins Rutenge.

2

Richard Rugimbana Mwenyekiti wa Chama cha Wanafunzi waliosoma katika shule ya (St Joseph Cathedral High School Alumn )kuanzia mwaka 1940 - 2014 akisisitiza jambo katika mkutano huo uliofanyika jana.

3

Mariam Ziaror mmoja wa wanachama hao akizungumza jambo wakati wa mkutano huo uliofanyika jana (St Joseph Cathedral High School .

4

Chief Edward Makwaia akichangia jambo katika mkutano huo

5

Bw. Hassan Ndumbaro mmoja wa wanachama hao akizungumza jambo katika mkutano huo kutoka kushoto ni Leaticia Mukarasa, Mariam Zialr na Chief Edward Makwaia.

6

Dr. Zubeida Tumbo kutoka taasisi ya Room To Read Tanzania ambaye pia alisoma katika shule hiyo akichangia mawazo yake wakati wa mkutano huo.

7

Baadhi ya wanachama wakiwa katika mkutano huo

9

Mkutano ukiendelea.

10

Mkuu wa shule ya (St Joseph Cathedral High School )Sr. Theodeta Faustin akizungumza na wanachama hao wakati wa mkutano huo.

No comments: