Social Icons

Saturday 20 December 2014

NEWS ALERT:MHADHIRI WA CHUO CHA TUMAINI TAWI LA MAKUMIRA MBEYA APATA AJALI MBAYA MCHANA HUU, MMOJA AFARIKI

Wakati Leo Mkoa wa Iringa unaadhimisha wiki ya usalama barabarani yenye kauli mbiu maamuzi yako barabarani ni hatima yetu - fikiri kwanza - Ajali mbaya msitu wa miti wa Mafinga Iringa mchana huu. Kwa mujibu wa habari zilizotikia aliyepoteza maisha ni Yunith Gwamaka Mwakenja ,majeruhi ni Dereva wa gari hilo ambaye nu mhadhiri wa chuo cha Tumain makumira Tawi la Mbeya Bw Gwamaka Mwakenja  pia  majeruhi mwingine ni Joyce Fredy. Wengine wametibiwa na kuruhusiwa. Chanzo inasadikika kuwa ni mwendo kasi na gari kuacha njia  kwa sababu ambazo bado hazijajulikana na kupinduka.

Chanzo Francis Godwin


No comments: