Social Icons

Tuesday 12 August 2014

MPYA MPYA: Nafasi za mafunzo ya utengenezaji wa mashine za kutotolesha Vifaranga vya Kuku.


OMARIBARAKA
Taasisi  ya  RafikiElimu  FOUNDATION  kupitia  MRADI  WA  ELIMU  YA  UJASIRIAMALI MIJINI  NA  VIJIJINJI  inatangaza  nafasi  za   MAFUNZO  YA  UTENGENEZAJI  WA MASHINE  ZA  KUTOTOLEA  VIFARANGA  WA  KUKU.
Mashine   zitakazo fundishwa  kutengeneza  ni  INCUBATOR   ( MANUAL & AUTOMATIC) ZENYE  UWEZO  WA  KUTUNZA  JOTO  KWA  SAA  48 PAMOJA  NA  KUTOTORESHA MAYAI   KUANZIA  240  HADI  5000.
Vile  vile  yatatolewa  mafunzo  ya   UTENGENEZAJI  WA  MAJIKO  SANIFU  NA  NISHATI MBADALA.
ADA   YA   MAFUNZO   :
Ada  ya  mafunzo  haya  ni  SHILINGI  ELFU  ISHIRINI  NA  TANO  TU. (Tshs.25,000/=)
TAREHE  YA  KUANZA  KWA  MAFUNZO
Mafunzo  haya  yatafanyika  kwa  muda  wa  siku  tano  kuanzia  tarehe    01  SEPTEMBA  2014 hadi  tarehe  05 SEPTEMBA  2014
FOMU   ZA   KUJIUNGA   NA   MAFUNZO :
Fomu  za  kujiunga  na  mafunzo  haya  zinapatikana  ofisini  kwetu  kwa  gharama  ya  SHILINGI ELFU  KUMI  NA  TANO  TU  ( Tshs.15,000/=).
MWISHO  WA  KUCHUKUA  FOMU  :
Mwisho  wa  kuchukua  fomu  ni  tarehe   28  AGOSTI 2014.
Ofisi  zetu  zinapatikana  katika  eneo  la  CHANGANYIKENI  karibu  na  CHUO  CHA TAKWIMU.
JINSI   YA   KUFIKA   OFISINI   KWETU
Kufika  ofisini  kwetu, panda  daladala za  UBUNGO- CHANGANYIKENI  kisha  shuka  kituo  cha TAKWIMU  halafu  tembea  hatua  ishirini  mbele  kisha  tazama  upande  wako  wa  kulia utaona ofisi  imeandikwa   RAEFO  TANZANIA.
Kwa  maelezo  zaidi wasiliana  nasi  kwa  simu 0784406508.
Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  mafunzo  ya  utengenezaji  wa  mashine  za  kutotolea  vifaranga, tembelea :

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.

No comments: