Frank
Mvungi_ Maelezo
Serikali imetoa fursa ya mikopo kwa wanafunzi
watakaojiunga na masomo ya stashahada maalum ya ualimu wa masomo ya Sayansi na
Hisabati.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari Elimu na Mawasiliano toka Bodi ya
Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya Juu Bw. Cosmas Mwaisobwa wakati wa Mkutano na
waandishi wa Habari Leo Jijini Dar es salaam.
“
Wanafunzi wapatao 5,000 wanatarajiwa kujiunga na stashahada maalum katika Chuo
Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambapo wote watanufaika na mikopo ya elimu ya
Juu.”Alisema Mwaisobwa
Akifafanunua,
mwaisobwa alisema kuwa lengo la mpango huo ni kusaidia kuondoa tatizo la walimu
wa masomo ya sayansi hapa nchini .
Aidha
Mwaisobwa alibainisha kuwa jumla ya maombi 58,037 ya mikopo yalikuwa yamepokelewa hadi kufikia Julai 2014
ambapo maombi 37,689 ni waombaji wa kiume na 19,592 ni waombaji wa kike.
Pia
Mwaisobwa alibainisha kuwa majina ya wanafunzi watakaopata mikopo kulingana na
udahili yatatangazwa kwenye tovuti ya Bodi ambayo ni www.heslb.go.tz.na taarifa hiyo
itatangazwa katika vyombo vya habari.
Bodi
ya Mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu (HESLB) inakusanya wastani wa shilingi
bilioni 3 kwa mwezi ikiwa ni marejesho ya mikopo iliyokwisha tolewa.
Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
No comments:
Post a Comment