Robert Otto
Mtangazaji AJ
Na vijimambo Blog
Robert Otto ni Mtanzania anayeishi Kansas City katika Jimbo la Kansas
nchini Marekani tangia mwaka 2007 na kama ada ya wageni wote wanaokuja
nchini Marekani kwa ajii ya kutafuta elimu na maisha bora, Robert Otto
ni mwenyeji wa Tarime mkoani Mara akitokea sehemu za Butuli na ni mtoto
wa kwanza kutoka kwa Mzee Thobias Otto.
Robert Otto kabla ya kuja Marekani aliendesha maisha na alipata elimu yake ya msingi ikiwemo elimu ya sekondari Dar es Salaam katika shule ya Azania na Tambaza na aliishi Keko juu na mwaka 1997 alifika nchini Marekani na alianzia maisha yake Brooklyn, New York na baadae akahamia Springfield, New Jersey na mwaka 1998 alihamia Wichita jimbo la Kansas na kujiunga na chuo cha Wichita State na kusomea computer engineering, electrical engineering, mathematics statistics na Nursing na alifuvu masomo yake 2005 na kubahatika kupata bachelor degree ya masomo yote na kuwa Best Student kwenye chuo hicho cha Wichita State.
Msome zaidi Bofya hapa>>>>>
No comments:
Post a Comment