Social Icons

Thursday 3 April 2014

INASIKITISHA SANA: MWANAFUNZI AUAWA KIKATILI KWA KUCHOMWA VISU NA MPENZI WAKE MBELE YA WAZAZI WAKE




Na Joseph Ngilisho, ARUSHA
SIRI nzito ya mauaji ya kinyama ya mwanafunzi wa Chuo cha Savanna Bridge cha jijini Arusha, Winfrida Akunay (18) aliyechomwa kisu mara sita eneo la shingo na kifua mbele ya baba yake mzazi imegundulika, Amani linakupatia.

Winfrida Akunay (18) enzi za uhai wake.



Kwa mujibu wa chanzo cha ndani, mtuhumiwa wa mauaji hayo, Robert Isaac (22) alitimiza ukatili huo nyumbani kwa baba wa marehemu Majengo Juu jijini hapa, Machi 25, mwaka huu, saa 2:12 usiku.

Ishu kubwa iliyojitokeza ni wivu wa mapenzi ambapo mgogoro mzito uliibuka kwa wawili hao.



Gazeti hili lilifuatilia kwa makini sakata la mauji hayo na kufanikiwa kupata waraka wa siri ulioandikwa na mtuhumiwa huyo ambapo sehemu ya waraka ilisema:


Mwili wa Winfrida Akunay ukiwa kwenye jeneza tayari kwa mazishi.



"Nakupa wiki moja ya kufikiria, kama utaendelea na msimamo wako wa kutokuwa na mimi nitakuua kwa mikono yangu mwenyewe na mimi kujiua." Mwenyekiti wa Mtaa wa Remtula, Majengo alisema baada ya mauaji hayo kesho yake walikwenda nyumbani kwa mtuhumiwa eneo la Ngusero alipokuwa akiiishi na mjomba wake na kufanya upekuzi chumbani ambapo walikuta karatasi iliyoandikwa:



"Mimi Robert Isaac nikiwa na akili timamu, nilikuwa na marehemu Winfrida kama wachumba kwa muda wa miaka miwili iliyopita, tuliahidiana kuoana baada ya kula yamini ya damu, lakini ilipofika mwezi wa pili, mwaka huu, marehemu alinikataa, lakini mwezi wa tatu tulifanikiwa kurejesha mahusiano mara tatu.”

Mwili wa Winfrida Akunay ukiombewa kabla ya kwenda kuzikwa.



GPL

SIKILIZA TONE RADIO HAPA LIVE
Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

No comments: