Social Icons

Wednesday 26 March 2014

CHUO CHA VETA CHATAMBULISHA MRADI WA USHIRIKIANO KATI YAKE NA UJERUMANI UJULIKANAO KAMA "GERMAN DUAL SYSTEM APPRENTICESHIP" JIJINI DAR


 Kaimu Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Dar Es Salaam VETA, Bi Benadetha Ndunguru akiongea na Waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano wa kutambulisha mradi wa ushirikiano kati ya Vyuo vya Ujerumani na VETA kwa wanafunzi wa Tanzania.
 Meneja Mradi wa "German Dual System Apprenticeship"(katikati) Martin Mac Mahon akizungumzia juu ya mradi ambao German wameshirikiana na Chuo cha VETA nchini katika kuhakikisha wanaboresha maswala ya elimu ya vitendo Tanzania. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Dar Es Salaam VETA, Bi Benadetha Ndunguru.
 Meneja Mradi wa "German Dual System Apprenticeship"(katikati) Martin Mac Mahon akiongea na waandishi wa habari wakati alipowatembeza kwenye moja ya karakana ambayo inatoa masomo kwa vitendo yaliyo chini ya mradi wa "German Dual System Apprenticeship" iliyopo katika Chuo Cha VETA kilichopo Chang'ombe jijini Dar Es Salaam.
 Meneja Mradi wa "German Dual System Apprenticeship"(katikati) Martin Mac Mahon akiwaonyesha moja ya magari yaliyotolewa na Kampuni ya Noble Motors kwaajili ya Mafunzo ya Vitendo yaliyo chini ya Mradi wa "German Dual System Apprenticeship" kwa wanafunzi wa Chuo Cha VETA.
 Wanafunzi wa Chuo Cha VETA wakiwa katika mafunzo kwa vitendo ambayo yapo chini ya mradi wa "German Dual System Apprenticeship" ambapo wanafunzi wanapata nafasi ya kufanya mafunzo kwa vitendo na kuunganishwa na makampuni ambao wanafunzi hao hupelekwa kwaajili ya mafunzo zaidi
Moja ya gari lililotolewa na Kampuni ya Noble Motor kwaajili ya mafunzo kwa vitendo yaliyo chini ya mradi wa "German Dual System Apprenticeship"
Moja ya gari lililotolewa na Kampuni ya Scania Tanzania kwaajili ya mafunzo kwa vitendo yaliyo chini ya mradi wa "German Dual System Apprenticeship"
 Kaimu Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Dar Es Salaam, Bi Benadetha Nduguru akiongea na waandishi wa habari wakati walipotembezwa kwenye moja ya karakana inayotumika kwaajili ya Mradi wa "German Dual System Apprenticeship"
Meneja Mradi wa "German Dual System Apprenticeship"(katikati) akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kuwatembeza waandishi wa habari na wageni waalikwa kwenye karakana zilizo chini ya Mradi wa "German Dual System Apprenticeship" ambapo Ujerumani na Chuo Cha VETA wameshirikiana katika mradi huo.
Picha na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

No comments: