Social Icons

Sunday 16 September 2012

MKUTANO WA WANAFUNZI AFRIKA MASHARIKI KUFANYIKA NOVEMBA 14



Mkurugenzi wa Mauzo wa Shirika la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini (AIESEC), Frank Mushi akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandhi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu mkutano utakaofanyika Nov.14-18. Kushoto ni Kiongozi wa maandalizi ya mkutano huo, Gwamaka Mwabuka na Rais wa AIESEC, Echo Wong
----
Na Shehe Semtawa


SHIRIKA la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini (AIESEC), litakuwa mwenyeji wa mkutano wa vijana zaidi ya 400 kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaozungumzia ushiriki wa vijana katika jumuiya hiyo.


Akizungumza na wandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo), jijini Dar es salaam leo, Msemaji wa Shirika hilo, Frank Mushi alisema mkutano huo utakuwa wa siku tano, kuanzia Novemba 14 hadi 18 mwaka huu.


Alisema mkutano huo unalengo la kuwajengea uwezo wa kujiwezesha katika shughuli mbalimbali za ujasiliamali katika jumuiya hiyo.


Mushi alisema mkutano huo ni wa sita tangu kuanzishwa shirika hilo miaka 13 iliyopita ambapo zaidi ya wanafunzi 35,000 wamenufaika kwa kujiajiri katika nyanja mbalimbali za kijasiriamali nchini.


“Katika mkutano wetu huo tutajadili namana ya kuzuia mchafuko vile vita ya dunia iliyopita, huko nyma, hivyo kukutana kwetu sisi vijana tutaweza kujifunza mambo mengi ya msingi na maedeleo katika nchi zetu”alisema Mushi.


Frank alizitaja nchi ambazo zitashiriki katika mkutano huo utakaofanyika jijini Dar es Saam ni pamoja na Kenye, Uganda, Rwanda, Burundi na wenyeji Tanzania.

No comments: