Social Icons

Wednesday 23 November 2011

DALADALA YA ITV YAFANA MKOANI MBEYA KUPITIA ZIARA YAO.

Wanachuo wa TIA Mbeya wakiingia katika Daladala, inayomilikiwa na kituo cha televisheni cha ITV katika ziara yao mkoani Mbeya hapo jana, ambapo wanavyuo hao walipata fursa ya kuweza kuchangia maoni yao kupiti mada zinazoendeshwa na kipindi cha Daladala kinachorushwa ITV kila siku kuanzia saa Kumi na mbili na nusu jioni hadi saa moja kamili usiku na watangazaji wawili Bi Kiroboto na Bwana Daniel Kijo.
Mtangazaji wa Kipindi cha Daladala kinachorushwa kila siku kuanzia Saa kumi na mbili na nusu hadi saa moja kamili usiku kupitia Televisheni ya ITV Bi Kiroboto akiwa ameketi katika kiti cha daladala wakati wa ziara yao mkoani Mbeya hapo jana.
Mtangazaji wa Kipindi cha Daladala kinachorushwa kila siku kuanzia Saa kumi na mbili na nusu hadi saa moja kamili usiku kupitia Televisheni ya ITV Bwana Daniel Kijo akiandikisha majina ya washiriki watakaongia maoni katika mada zinazoendeshwa na kipindi hicho, katika ziara yao mkoani Mbeya hapo jana.

No comments: