Hakuna upendeleo hapa kila mtu yupo na kazi kubwa ya kuchambua na kuhakikisha anapitia vizuri fomu zaidi ya 4,000 za ushiriki wa Maisha Plus/ Mama shujaa wa chakula
Mmoja ya wa wanachuo akihakikisha mahesabu kama ametoa alama sahihi kabisa wakati wa zoezi hilo la kuchuja na kupitia fomu za washiriki wa shindano la Maisha plus/ Mama shujaa wa Chakula
Kwa umakini kabisa Kila mmoja anafuatilia na kuangalia fomu kwa umakini wakati wa kuwatafuta wale watakaoingia katika usahili
Mmoja ya wanachuo akifanya mapitio kwa kusoma kile kilicho andikwa na moja ya fomu za washiriki.
Baadhi ya wanachuo wakiwa wanasahihisha kwa umakini Fomu za washiriki na kuzipitia ili watende haki wakati wa mchujo huo ambapo Fomu hizo baada ya hapo zinatoka moja kwa moja hadi kwa majaji wakuu ambao hawapo pichani.
Kazi ikiwa inaendelea kwa umakini
Mmoja wa wanachuo akitafakari Jambo wakati wa kufanya zoezi la Mchujo
Kazi zinaendelea
Mmoja ya wanachuo wa kwanza kulia akimalizia kuhakikisha alama zake katika 'notebook'
***************************
SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA/ MAISHA PLUS
- Fomu zaidi ya 4,000 za Mama Shujaa Maisha Plus zakusanywa
- Majaji 9 kusimamia zoezi la kuchaguwa wakulima wanawake 20 na vijana 45
Zoezi la kuchaguwa washiriki wa
shindano la Mama Shujaa wa Chakula na Maisha Plus limeanza leo ambapo zaidi ya fomu 4,000
zimekusanywa kutoka kwa washiriki.
Eluka Kibona, Meneja
Utetezi na Ushawishi wa Oxfam akiongea wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo alisema
zoezi la kupitia fomu litachukuwa siku nne kuanzia Jumatatu tarehe 3 hadi
Alhamisi tarehe 6 Februari 2014. “Majaji
walioteuliwa wana kazi kubwa ya kupitia zaidi ya fomu 4,000 ambazo tumekishwazipokea
na nyingine bado zinawasili kutoka sehemu mbalimbali za nchi yetu. Baada ya
uchambuzi majaji watachaguwa wakulima wanawake 20 pamoja na vijana 45 ambao
watashiriki kwenye shindano la mwaka huu. Majaji watasaidia kuchambuwa fomu na
vijana 17 waliojitolea kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitengo cha Jinsia.
“
Jopo la majaji linajumuisha
waliobobea kwenye masuala yanayohusu kilimo, ufugaji, usalama wa chakula, sera
na utetezi, uchumi, biashara, vyombo vya habari, vijana na maendeleo ya jamii.
Majaji ni
kama wafuatavyo:
Rose Tesha Meneja
Programu ya Maisha Salama shirika la VSO; Masoud Kipanya mwanzilishi wa shindano
la Maisha Plus; Tatu Abdi Juma mshindi wa tatu shindano la Mama Shujaa wa
Chakula 2012 ; Francis Bonda Mkurugenzi wa kampuni ya DMB na mwanzilishi
wa shindano la Maisha Plus, Edmund Matotay Mtafiti kutoka shirika la Oxfam; Anna Oloshoro mshiriki
wa shindano la Mama Shujaa wa Chakula mwaka 2011; Carolyn Kandusi mtaalamu wa
jinsia kutoka shirika la PINGOS akitokea Loliondo; Zephaniah Mugittu mshauri
wa mnyororo wa thamani wa mboga mboga anafanya kazi na shirika la Oxfam akitokea
Lushoto, Tanga pamoja na Bernick Kimiro mshindi wa Maisha
Plus 2012.
Washiriki
wa Maisha Plus msimu huu ni vijana wa miaka 21-26 kutoka nchi za
Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda wanaogombania kitita cha
Fedha za kitanzania Milioni 25.
No comments:
Post a Comment