Social Icons

Wednesday 8 July 2015

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA IRINGA CHAMPONGEZA ELISHA MWAMPASHI KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA KATIKA JIMBO LA IRINGA MJINI‏

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.



katibu wa jimbo la iringa mjini ELISHA MWAMPASHI
katibu wa jimbo la iringa mjini ELISHA MWAMPASHI
 KEKI ILIYOKUWA IMEANDALIWA SIKU YA SHEREHE HIYO.
 Baadhi  ya wanachama wa chama cha mapinduzi tawi la chuo kikuu cha iringa zamani tumaini.

 NA FREDY MGUNDA,IRINGA

Baadhi  ya wanachama wa chama cha mapinduzi tawi la chuo kikuu cha iringa zamani tumaini wamefanya maafari yao katika ukumbi wa chama hicho sabasaba.

Wakizungumza wakati wa sherehe hiyo wanafunzi hao wamesema kuwa sas ccm italajia kurudisha jimbo la iringa mjini kwasababu tayari makatibu wa chama hicho wameweza kuwarudisha vijana kukipenda chama hicho.

Aidha wamesema kuwa  chama hicho kilipoteza mvuto kwa vijana na vijana walipoteza mvuto na chama hicho,hivyo chama hicho kwa sasa kimerudisha  imani kwa vijana na wanachama wengine.

“Sisi hapa chuoni kwetu tulikuwa wanachama  wachache ila kwa sasa tupo wengi na kila siku wanachama wanazidi kuongezeka kutokana na kukipenda cha hicho kwa wakati huu tukielekea katika uchaguzi mkuu”walisema wanafunzi hao.

Mbunge wa jimbo hili kwa sasa mchungaji PETTER MSIGWA ajiandae kuondoka kutoka na chama hicho kujipanga kila kona na tayari wamejihakikishia ushindi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu na kuongeza kuwa wananchi wa manispaa ya iringa wanapenda amani na sio vurugu.

Lakini walimpongeza katibu wa jimbo la iringa mjini ELISHA MWAMPASHI kwa kufanya kazi  nzuri iliyosababisha wananchi wa jimbo hili kurudisha imani na chama hichi na kuongeza kuwa MWAMPASHI ni kiongozi mzuri na anajua majukumu yake hivyo ni vizuri wananchi wa manispaa tukashikiana na jembe hili kulikomboa jimbo hili.

Kwa upande wake KATIBU WA JIMBO HILI ELISHA MWAMPASHE ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hiyo aliwapongeza wanachama wa chama hicho tawi la tumaini kwa kukikuza chama hicho na kuongeza wanachama.

MWAMPASHI akawataka wanachama hao kukipigania chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao ili waweze kushinda kwa kishindo kikubwa na kuwaachawapinzani hoi.

“Tunanguvu na nia ya kufanya vizuri katika uchaguzi wa mwaka huu kwa kuwa tumejipanga kili kona na tumerudisha inmani kwa wananchi wote hivyo kazi kwa sasa imekuwa rahisi hasa kulikomboa jimbo la iringa mjini ambalo walilikopesha kwa mpinzani”alisema MWAMPASHI.

Aidha MWAMPASHI aliwataka wananfunzi kuacha kufanya mambo ya kizinaa pindi wapatapo kazi kwa kudai kuwa anakura ujana ,akaongeza kuwa sasa ni wakati wa vijana kuwekeza katika biashara mbalimbali ili kujitengenezea maisha mazuri hapo baadae.

“Nawaomba jamani tusiwe na tamaa katika kutafuta maendeleo kwa kuiba au kutoa na kupokea rushwa  kwa kuwa hiyo njia sia sahihi kwani hapo mtakuwa mkirudisha maendeleo nyuma na sio kuendelea kuleta maendeleo”.alisema MWAMPASHI.

Alimalizia kwa kumtaka mbuge wa jimbo hili kufungasha vitu vyake kwa kuwa muda wake umeisha na wananchi wa manispaa ya iringa wamemchoka kwa kuwa toka ameingia madarakani hakuna alichokifanya katka kuleta maendeleo ya jimbo hili zaidi kuanzisha migomo na vurugu katika sehemu mbalimbali.


No comments: