Social Icons

Thursday 10 September 2015

WADAU WA ELIMU JUU KUKUTANA JIJINI ARUSHA.‏

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

JenikisaNdile – MAELEZO
10/09/2015. Dar es salaam.

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeandaa Kongamano la siku mbili la Elimu ya Juu litakalofanyika jijini Arusha kwa lengo la kuwa na jukwaa la kubadilishana uzoefu na maarifa miongoni mwa wadau wa elimu nchini.
Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) Prof. Yunus Mgaya alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam .

Amesema Kongamano hilo litaenda sambamba na Maonesho ya shughuli mbalimbali zikiwemo za utoaji wa huduma, na maonesho ya bidhaa mbalimbali kuonyesha mafanikio ya elimu  yaliyopatikana nchini.
Amesema washiriki wa mkutano huo kutoka taasisi mbalimbali watapata fursa ya kuchangia miradi elimu kwa ili kuinua sekta hiyo hapa nchini.


BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI>>

No comments: