Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi.
Beng’i Issa akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu hapa nchini (hawapo
pichani) wakati akifunga mafunzo ya wiki nane ya ujasiriamali kwa
wanafunzi hao mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mafunzo hayo
yaliendeshwa chini ya mpango wa Cambridge Development Initiative (CDI)
ili kuimarisha mafunzo ya maswala ya ujasiriamali kwa wanafunzi wa vyuo
vikuu hapa nchini. CDI ni mpango ulioasisiwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu
cha Cambridge cha nchini uingereza. Kulia ni Rais wa CDI, Ravi
Solanki.
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi.
Beng’i Issa (katikati) akikabidhi hundi ya dola 3000 kwa wanafunzi
wawili kutoka chuo kikuu cha Ardhi walioibuka washindi kwa wazo bora la
biashara baada ya mafunzo ya wiki nane ya ujasiriamali yaliyoendeshwa na
NEEC kwa ushirikiano na mpango wa Cambridge Development Initiative
(CDI) unaoendeshwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Cambridge cha nchini
Uingereza. Wengine ni Moses Mtei, mshindi (kushoto); Mkurugenzi wa
Ujasiriamali CDI, Bi. Georgia Ware (kulia); na Joel Kissava pia mshindi
toka Chuo kikuu Ardhi (wapili kulia). Hafla hiyo ilifanyika mwishoni
mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi.
Beng’i Issa (wa pili kushoto) akikabidhi hundi ya dola 3000 kwa mmoja
wa wanafunzi walioibuka washindi kwa wazo bora la biashara baada ya
mafunzo ya wiki nane ya ujasiriamali yaliyoendeshwa na NEEC kwa
ushirikiano na mpango wa Cambridge Development Initiative (CDI)
unaoendeshwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Cambridge cha nchini
Uingereza. Wengine ni Bhoke Nyaisaba toka UDSM, mshindi (kulia);
Mkurugenzi wa Ujasiriamali CDI, Bi. Georgia Ware (wa pili kulia); na
mwanafunzi toka UDSM, Vivian Mushi (kushoto). Hafla hiyo ilifanyika
mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment