Social Icons

Friday 23 January 2015

Ujenzi Chuo cha Tiba Mloganzila kugharimu zaidi ya Dola za Kimarekani Milioni 61

Wewe ni Mwanachuo? Tuwasiliane kwa namba 0654221465

Na Anitha Jonas – MAELEZO.

SERIKALI imesema kuwa mradi wa ujenzi wa  Chuo cha Tiba  cha Kimataifa cha Muhimbili  eneo la Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es salaam utagharimu kiasi cha Dola za kimarekani Milioni 61.

Katika mradi huo serikali yTanzania imechangia dola za kimarekani milioni 18 na serikali ya Jamhuri  ya Korea imetoa mkopo wa dola za kimarekani milioni 43 ili kufanikisha ujenzi wa chuo hicho katika eneo la Mlonganzila jijini Dar es Salaam.

Akizungumza  mara baada ya kukamilisha  ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa chuo hicho jana jijini Dar es salaam Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi  Dkt.Shukuru Kawambwa  alisema kuwa mradi huo na  unatarajiwa kukamilika mwezi  Machi mwakani.
“Tumejipanga vizuri  kujenga  Chuo hiki cha Tiba ambacho kitakua mji wa tiba hapa nchini, sisi kama serikali tumeiona changamoto ya wataalam wa afya nchini na kuona ni vyema kujenga chuo cha kisasa kitakachokua na uwezo wa kupokea  zaidi ya wanafunzi 15,000  kwa mwaka watakaosaidia kuondoa tatizo la wataalamu wa afya.” alisema Dkt.Kawambwa.

 Dkt. Kawambwa alisema kuwa mbali na ujenzi wa chuo hicho, serikali itajenga hospitali nyingine ya Muhimbili ambayo ujenzi wake utamalizika sambamba na ujenzi wa chuo hicho ili kuwawezeha wananchi kupata huduma bora za afya.

Alibainisha kuwa  hospitali hiyo pindi itakapokamilika itakuwa kubwa zaidi  na yenye vifaa vya kisasa  itakayosaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa uliopo katika hospitali ya Taifa Muhimbili pamoja na kuwasaidia wanafunzi kupata sehemu ya mafunzo kwa vitendo.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha Tiba Muhimbili Prof. Ephata  Kaaya  alisema mradi huo umegawanyika katika awamu mbili, awamu ya kwanza ikihusisha  ujenzi wa chuo cha tiba na Hospitali ya kisasa ya muhimbili na awamu ya pili  itakuwa ujenzi wa hospitali  kubwa ya kutibu magonjwa ya Moyo na mishipa ya fahamu.

“ Tayari Benki ya Maendeleo  Afrika imetoa  kiasi cha zaidi ya dola za kimarekani milioni 9 kwa ajili ya ujenzi  wa Chuo  na hospitali ya kimataifa ya magonjwa ya moyo na mishipa ya fahamu itakayokuwa na ubora wa hali ya juu katika nchi za Afrika Mashariki” alisisitiza Prof.Kaaya .

 Aliongeza kuwa gharama ya vifaa tiba ikiwemo vya uchunguzi na upasuaji utagharimu zaidi ya dola za kimarekani Milioni 27 na kueleza kuwa mkandarasi wa kufunga vifaa tiba vya mradi huo ameshapatikana  na anatarajia kuanza kufanya kazi hiyo hivi karibuni.


Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.

No comments: