Social Icons

Monday 13 October 2014

PSPF YATOA MSAADA WA KOMPYUTA 12 KWA VYUO VIWILI BAGAMOYO

 Afisa Mahusiano wa PSPF Coleta Mnyamani kushoto Akimkabidhi Msaada wa Kompyuta Mkuu wa Chuo Kikuu teule cha Marian Father Luke Mbefo  ambapo Kompyuta hizo zitatumika katika Kuhifadhi Nyaraka mbalimbali za Maktaba
 
 Mkuu wa Chuo Kikuu teule cha Marian Father Luke Mbefo  kulia akimshukuru Afisa Mahusiano wa PSPF Bi. Coleta Mnyamani kwa msaada huo
 Mwakirishi wa Shirika la Roho Mtakatifu Father Nicetas Kyara akitoa neno la Shukurani Baada ya kukabidhiwa msaada wa Kompyuta Mbili za kisasa kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF
 Afisa Mahusiano wa PSPF Bi. Coleta Mnyamani akizungumza neno Baada ya kukabidhi Msaada huo
Afisa wa Fedha kutoka PSPF Bwana Samwel Haule Akizungumza Jambo wakati wa Makabidhiano wa Kompyuta hizo katika Chuo Kikuu teule cha Marian
 Mkuu wa Chuo teule cha Marian Father Luke Mbefo wakiteta Jambo na Afisa Mahusiano wa Pspf Bi Coleta Haule Baada ya Kukabidhi Msaada huo
 Picha ya Pamoja ya Viongozi wa PSPF na Chuo  Kikuu teule cha Marian
Kulia ni Meneja wa Pwani wa PSPF Msafiri S. Mugaka akimkabidhi Kompyuta 10 Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Ukutubi,Uhifadhi wa Kumbukumbu na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania Dkt. Ally S. Mcharazo kwa niaba ya chuo hicho
Meneja wa Pwani wa PSPF Msafiri S. Mugaka  akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Ukutubi,Uhifadhi wa Kumbukumbu pamoja na wagani waalikwa wakati wa kukabidhi msaada huo wa kompyuta 10 za kisasa
Rais wa Chuo cha Chuo cha Ukutubi,Uhifadhi wa Kumbukumbu Daudi Joho akitoa neno la Asante Baadhi ya Kukabidhiwa Msaada huo 
Mbele ni Maofisa wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Ukutubi,Uhifadhi wa Kumbukumbu na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania Dkt. Ally S. Mcharazo  akitoa neno la Shukurani
 Baadhi ya wanafunzi wakisoma Vipeperushi vya PSPF
Wanafunzi wakiwa wanafuatilia kwa makini
Kila mtu anachukua Kumbukumbu


Mfuko wa pensheni wa PSPF waendelea kukuza elimu ya Tehama katika vyuo mbalimbali hapa nchini kwa kutoa msaada wa jumla ya kompyuta 12 katika chuo cha Ukutubi Uhifadhi wa Nyaraka Bagamoyo na chuo Teule  ambacho kitakuwa kikiendeshwa chini ya saint augustine's university  (SAUTI) ambapo  kompyuta kumi (10) zimetolewa  katika chuo cha Ukutubi Uhifadhi wa Nyaraka na Mbili zimetolewa katika chuo teule cha cha Mariana university College vyote vilivyopo bagamoyo katika mkoa wa pwani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo afisa mahusiano wa PSPF Bi. Coletha Mnyamani amesema zoezi hilo limeanza lakin halitaishia hapo kwani ni zoezi endelevu kwani wameamua kusaidia jamii hususani kwa wanafunzi ilikuweza kuwajengea ujuzi katika masomo yao pamoja na kutunza nyaraka zao kisasa na sio katika makaratasi  kama ilivyo kuwa hapo zamani

Kwaupande wake Meneja wa  Wa PSPF Mkoa wa Pwani  Bw.Msafiri S Mugaka amesema kuwa wameweza kutimiza ahadi waliyo ahidi kwa chuo cha Ukutubi Uhifadhi wa Nyaraka na kuweza kutoa msaada kwa chuo teule cha Mariana university College Hivyo wawaomba wananchi kuiamini na kuendelea kuwa wanafamilia wa mfuko huo wa pensheni

Naye Mwenyekiti wa Baraza la chuo cha Ukutubi Uhifadhi wa Nyaraka na mkurugenzi wa wa Bodi ya Huduma za Maktaba –Tanzania Ally  Mcharazo kilichopo Bagamoyo wakati akipokea msaada huo kutoka kwa maafisa wa mfuko wa PSPF makao makuu Dar es saalam Amesea wanatoa shukrani kwa Mfuko huo kwani umeweza kuwasogeza katika huduma za kisasa kwa kuwapelekea kompyuta hizo nyaraka zote zitakuwa zikitunzwa katika hali iliyo salama na sio katika hali ya kizamani na kazi kuenda kwa haraka zaidi kwani kompyuta husaidia katika kuokoa muda kazini.

Pia Bw.Samweli Haule ambaye ni afisa Wa Fedha Wa Mfuko Wa Pensheni wa PSPF Aliweza kutoa maneno ya kuwaasa wanafunzi kwa kuwa makini na wao hawata choka kutoa msaada pindi wanapo kuwa wamekwama ili kuweza kuwaweka wanafunzi wote katika hali ya kisasa zaidi

Mkuu wa Chuo cha Mariana university College Father Luke Mbefo pia naye aliweza kushukuru Mfuko wa PSPF kwa kuona umuhimu wa kuweza kusaidia upande wa elimu kwa kuchangia kwa aina mbalimbali bila kuchoka na kuchagua rangi wala dini

Hivyo Mfuko wa Pensheni PSPF Umetoa wito kwa wananchi  pamoja na vyuo mbalimbali kwakuwa wao wapo kwamoyo kwaajili ya wananchi na kuhakikisha kuweza kuikomboa elimu yetu kwa kuipelekea wepesi zaidi katika hali ya udigitali kuachana na analogia,kwani huop ni mwanzo tu mambo mengine yatafuata tena mazuri kutoka PSPF


Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.

No comments: