Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam (UDASA), Imeandaa Kongamano la kujadili mchakato wa kupata Katiba
mpya ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Kongamano hilo litafanyika
tarehe 27 Julai 2014 siku ya Jumapili kuanzia saa 8 mchana ndani ya ukumbi wa
Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kongamano hilo litarushwa moja kwa
moja na kituo cha televisheni cha Star TV
Mada kuu ya kongamano hilo ni, “Tujadili na Kutafakari
Mchakato wa Katiba Mpya kwa Manufaa ya Taifa Letu”.
Watoa Mada katika kongamano hilo ni Prof. Y. Msanjila na Dkt. Kitila Mkumbo
Tunapenda kuchukua fursa hii kwa heshima kubwa
kuwakaribisha wananchi wote ili wawe miongoni mwa watu watakaotoa mchango wao
mkubwa katika mchakato wa kuleta maridhiano ya kitaifa kuhusu upatikanaji wa
Katiba Mpya ya taifa letu la Tanzania.
Tutanguliza shukrani zetu za dhati kwa ushiriki wako
kwenye kongamano hili.
Imetolewa na
Bw. Faraja Kristomus.
(Katibu – UDASA)
0787 52 53 96 / 0717 086 135
Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
No comments:
Post a Comment